Tunahitaji kumjua Mungu sana, Ayubu 22:21 maandiko yanasema mjue sana Mungu ili uwe na amani ndipo mema yatakujia,haya yooote ni shetani yuko kazini anatuvuruga,roho ya mauti mara ajali mara magonjwa mara kuchomana visu ni mauti,mauti. Lakini tunao mwamini Yesu hatuachi kuzijua hila za adui,shetani anafanya kila mbinu kuvuruga kusudi la ndoa,familia. Hapa anashangilia Watoto wateseke, Baba kafa,Mama kafungwa!! Mungu turehemu 🙏
Mwanamke mwenye hekima hujenga nyumba yake mwenyewe bali mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe. Tayari ametengeneza laana ya damu kwa mikono yake mwenyewe na mtaka yote kwa pupa hukosa yote. Familia iwasaidie hao watoto kuvunja hiyo laana maana itawatafuna mpaka kizazi cha 4. Damu ya mtu kuimwaga chini lazima idai tu. Kama Kaini na Abeli. Tutafakari sana wanawake kabla ya kutenda.
Hili jambo ni chungu kila upande. Hatujui mengi. Hatujui walianzaje maisha yao hadi hapo walipokuwa wamefikia. Hatujui nyumba ndogo iliingiaje kwenye maisha yao, ni pepo? Ni nini? MUNGU tu atusaidie
Duh poleni waombolezaji but nimekubali Sana diwani he is of Justice and anajua anachokifanya let us join together to make sure that these evils are not be continuous 🙏
Ukiwa na hasira huwezi kufanya maamuzi sahihi ndio maana tunasikia matukio kama haya. Tunajudge sana kwa sababu hayajtufika lkn likikukuta cha kufanya kinajulikana hapohapo. Mwenyez mungu atusaidie
@@annasolomon9855 my dear kuna situations ni ngumu unaweza kupitia na kama huna watu wa kukaa nao karibu you can kill anyone. Everyone is capable of killing someone trust me. Kama hujapitia hii situation huwez kuelewa na muombe Mungu asikupitishe huko.
Diwani taratibu hayakufika omba Mungu yasikufike, usiwe mkali hujui yule Mama yaliyomfikisha hapo, acha Serikali ifanye kazi yake, kutetea michepuko unaharibu kujengewa nyumba sio ruhusa ya kwenda kuchepuka
Embu nyamaza we mtu.. unajua maana ya mtu kufa? Kuna njia nyingi za kufanya kama mtu ameamua kuwa na mchepuko sio kumuua mtu , kifo ni kitu tofauti usiongee .. hata kama amefanyia Nini huwezi linganisha na kifo aisee we vipi .. haya yatokee kwa kakako na babako ndo utajua hujui
Nyumba ni nn wewe? Kuna mwanaume asiechepuka?? Labda awe na tezi dume au sukari. Wivu wa kijinga angekuwa kaka yako ameuliwa ungesema hivyo? Hata km amemtoa wapi aisee
Waswahili wanasema ajuae mdundo wa ngoma ni aliyecheza ngoma sisi tutaongea sana na kuhukumu sana lkn mwisho wa siku hatujui huyu mama alikutana na maumivu gani akashindwa kujizuiya kwenye ndoa kuna mengi majambo na nyie wanaume hatusemi msichepuke coz wanawake wako wengi na wataenda wapi tatizo dharau nyumbani za nini si mchepuke kwa heshima
Lakini Sensa haionyeshi wanawake kuwa wengi hivyo tofauti ni 1m Tu kila mwanamume akisema awe na wawili maana yake watanyakanyana wanawake. Labda useme wanawake wanapenda penye mshiko ndio mana wanaolewa wote sehemu moja😅
Huyu muuwaji hajawaji kutoka na mwanaume mwingine? Mpaka amtoe roho mtoto wa watu. Aliolewa akiwa bikra. Vitabu vya Mungu vinatufundisha kusamehe kama tunavyosamehe wanaotukosea. Kwanini sasa tunaendekeza hasira za kipumbavu? Atiwe ndani na sheria ichukue mkondo wake na soon ahukumiwe. Wenye akili ya kuuwa mtu kwa sababu ya mapenzi bila hata huruma ya kutambua mchango kwa maisha ya familia walaaniwe.
Kwa mwonekano wake hajatulia inaonyesha ni wale kina mama wanaopenda kuwa juu ya waime zao kisa ndao na mwanaume akaliruhusu Hilo nawasii sana wanaume waishi na ss kwa akili kama maandiko yanavyosema
Huyu kabla hajanyongwa abanwe kwanza atujuze ni nani yuko nyuma yake tunasikia Kuna mashoga zake walikuwa wanampaplish na sim zao zichunguzwe wakibainika na wao watakuwa wameshiriki mauaji wote nyongelea mbali
@@lidyakisoka-is4ru nilishamuona kwenye msiba wa yule mtt ameuwa mama yake na kumzika aliongea ujinga Sana mpaka Mh tulia akasema waachie serikal, wamchunguze huyo diwan kwa maneno yake tu uwenda kashauza viwanja vya watu sana
Huyu Diwani nawasiwasi kaone hai wtt wa kike isije kuwa anawatamani eti watt sio Lazima waishi na bb au mama mara ndugu wa upande wa pili wasiulize kuhusu wtt anataka kuwabaka au,kwanza yy sio mkibosho ni mpare Wamsele kuweni makini mtapoteza na watt
Nina nyumba,nina watoto,natembelea prado??nimfuateeee mtu sijui wapi huko eti hadi nichome kisu??niwaache wanangu,nyumba yangu nikaozee jela???Mungu tupe hekima tutambue mambo yote ya hii dunia ni ubatili mtupu na kujilisha upepo.....hawa watoto hawataweza kumuelewa mama yao hata cku moja,,kheri nusu shari kuliko shari kamili 😭😭😭
Mimi nasema apana ata km anawanake 20 nyumba nzuri umejengewa wtt 6 umezaa nae alafu uyo mchepuko sio km kakutoa ww akamleta mchepuko ww upo kwenye nyumba yk shida ipo wapi tufike wakati wanawake tujitambue ss apo amepata faida gani mume kamuuwa yeye yuko ndani ata hao wtt sidhani km watakuwa na imani tena na uyo mama yao japo mzazi ni mzazi
Huyo mama pengne ata Mia take ilikua sio kuua jaman msimseme Sana ata huyo mwanaume ndio ilikua chanzo kakaa kwenye ndoa take miaka yote hiyo mwisho wa siku anakua msaliti inauma Sana kwakweli
Kizazi cha Kaini cha kuua, hiyo ni laana mbaya sana hata watoto wake watamchukia mama yao sana, hiyo familia imtafute Mungu sana na kutubu hiyo laana ya kumwaga damu isamehewe
Kwa kweli mwanamke alikusudia kabisa pomwani ni mbali sana alijiandaa, Na wakati mume kamjengea nyumba nzuri na watoto 6 na anapata anachokihitaji chuki yote hiyo ya nini kwa kweli hata mimi sikubaliani nae, wivu au ni muuaji huyo 😊
kwani kwao hakuacha nyumba? kwani alifuata nyumba hapo... kujengewa nyumba sio ndio ruhuza kuwa na mke mwingine. Abadili dini awe muisilamu basi..Na hiyo kanisa inamzikaje mzinzi? Au kwa vile alikuwa anatoa Sadaka? Double standards... shame on you church!!!! wote wamevunja amri za Mungu. Mmoja kazini ila kasababishia mwingine kuuwa. Wote wanadhambi. Lakini asingezini asingeuawa!!!!.Nani kaanza kosa hapo??
Hakufuata nyumba wala Magazine bali ALIUFUATA UPENDO WA KWELI AMBAO MWANZO ALIMPATIA NA SASA AMEUMEGA NA KUPELEKA KWA MPANGO WA KANDO ,HILO NDO TATZO..
Amri ya Mungu " usiue ". Je mama amempata yule mume ? Je mama kaua mume, sijui pilato atampa hukumu gani,- alitafakari kuwa baada ta kuua mume,nani atalea hao watoto wao maana baba kaua na yeye atasota jela ? Hasira za mkizi a. Atakosa vyote
Kwann mwanaume anajihangaisha na mwanamke mwingne???kama hamtaki huyo mama angemwambia ukweli kama hamtaki,wanaume acheni kuhangaika na michepuko au basi basi dini iruhusu kuoa mwanamke zaidi ya mmoja.
Pole sana mpendwa, angekua kaka yako, au mwanao ungesema hivyo? Ni mwanaume yupi umjuae ni mtakatifu? Kabla hatujahukumu tujitafakari ni nani aliye safimwenzio akinyolewa tia maji, hajawahi kutenda dhambi?
Tena hawawezi mnyonga na alipelekwa mochwari kuaga mume wake ahakikishe ni yeye atakaa ndani ila Iko ck atatoka akalele watoto wake Sasa nani km mama hakuna hata awe mbaya hata awe mchawi utamfanyaje na ndo mzazi wako inauma ila hamna njia tunaongea tuu
Hapo Mungu asimame kwa kweli Ndio mwanzo wa watoto kusambaratika maskin😢.....diwan upo sawa lkn hujawafikiria watoto 6 alafu bado wadogo jamn wanakuwa mayatimaa
Anaewatuma mchepuke nan?! Hamjui mama amepitia nn pak kufany ivyo n hzo n hasira tu wew unatetea kwasababu n ww n mchepukaj t.Dear women ukiona red flags km hiz za wa chepkaj kimbia so lazma mzeeke wote
Hakuna mwenye haki ya kuua.Huyo angaliom a talaka tu na siyo kuua 😢😢Ni muuaji na mjinga mkubwa sana.Anamuua baba wa watoto sita 😢😢Aibu pia kwa wanawake wote 😢😢
Huyu diwani ni chenga anauhakika gani kama huyo mwanaume ndie aliyejenga hiyo nyumba????ndoa zina siri nyingi.Niko kufikiri mwanamke hawezi kujenga.Hivi hamumunio rais na spika na wengine wengi nao wanajengewa???fikra finyu
We ni diwani tuu.ya ndoa huyajui.amazaa watoto 6 na nyumba nzuri nio cheating cha kumsaliti?? Wanaume walindwe kkwa kosa la malandokando.acha usiisaidie serikali ina macho pale palikuwa na mke na mc hepuko mlijuaje muuwaji?? Wakamatwe wote wawili wakajitetee mahakamani ..
Wanawake wa Moshi Mimi nawaogopa sana maana matukiyo kwenu yamekuwa mengi sana mala kuuwa wazazi Kisa Mali mala muuwe wame zenu namengineyo mengi njiee TU duuuu
Hapo huyo mwanaume angeleta Ukimwi nyumban hakuna mtu angeleta mdomo me namuombea huyo Mwanamke Mungu amsimamie atoke alee wanae na wanaume muache michepukoooo
Tunachojua kila mtu alikosea ila hakuna anaejua hali halisi ya hiyo familia zaidi ya Mungu. Na mimi namuombea huyo mama atoke alee watoto wake. Siri ya familia aijua mke na mume na sio majirani jamani😢
Mapenzi yanauma sana hasa pale unapojua mwenzi wako muda huu anagawa utamu ambao ungependa uupate peke yako, maumivu yake sio mchezo, halafu ukute mwanaume hakupendi tena kahamishia mapenzi kwa mchepuko na anaondoka muda wowote anaojisikia bila kujali, ukimwambia haelewi anakuona kama kinyago, aiseee roho inafurukuta sana ni bora mtu achepuke halafu akuheshimu awe anajiiba kwenda, sio kwenda huku mkewe anajua na anaona huwezi mfanya chochote, haya ndio malipo yao pumbavu
Usiombe yakukute wmanaume akipata mchepuko make wandani ana kuwa mavi mkewako amekuzaliya watoto wazuri namnahiyo Bado unataka nini ulichokitaka umekipata Mungu atakusaidia mwanamke mwenzangu utatoka
Kuna watu wana uelewa mdogo wa mambo na wameshikiwa akili na mifumo ya sasa tulioletewa na wazungu. Magonjwa yameletwa ma wazungu na hata hivyo haiwezi kuwa kigezo cha kumuua mwenzako.
Kuuwa kakosea ssna ila kwnn wanaume amtulii eti.kamjengea nyumba na wtt 6 ..no nyumba wamejenga pamoja hili waishi kujenga familia yso busna wanaume acheni kutngatangaa buana..ila mauji si maxuri atua ichukuliwe lakini wanaume madababisha vitaa mnaumiza wamama mkiwa na pesa mikia juu mkiwa na dhiki mke ndio mkeoo mkipata tuu mnakimbiaa acheni buana nyiee
Hakuna hasira hapo alidhamiria na sio yeye pekeyake kuna watu nyuma yake,ni tukio limepangwa siku nyingi,huwezi toka nyumbani kwako na kisu useme ni hasira.
Juma, we ni mbunge wa moshi ujae,hukurupukag, Ungeendela kua mayor, kipande cha barabara kutoka matindigan, MPESA kwenda Shabaha kingekarabatiwa, sio kwa mateso tunayoyapata
❤kina mama tulieni nyumbani .leeni watoto ,acheni wivu wa kipimbavu.unamfatilia ulimuumba wewe?? Unafatilia nini? Wewe ni mkamilifu !?? Kwanini uwakatili watoto Baba yao kwa sababu ya Mawivu yako ??? Unajikuta wewe ni nani!?? Wewe ni taka taka kama taka taka zinqine.pyuuuui
Mnajua kuongea sana kwa vifungu vya sheria kabisa mwanaume akiua hapo utasikia wivu wa mapenzi muwe mnatulia kazi iendelee sa ivi mtaipata habari yenu kwani nyie mnavyoua wanawake zenu huwa watoto wanabaki na nani???
Nashangaa sana wanaume wanavyofoka, hivi ni wanawake wangapi wanauawa na wanaume kwa mwezi, mbona hatusikii hizo kelele?? Yule Saidi wa Mwanza alimuua mke eti kwa sababu hakupokea simu alivyoenda kwa mama yake, huyu diwani mbona hakufoka. Zinaa ina malipo, ndio hayo yaliyomkuta Mr marehemu. No mercy for cheating husbands.
Ila jamani tujuangalie na tutafakari sana kwakila unalokusudia kumtendea mtu sasa umemuua mumeo sawa wewe unaishia gerezani watoto hao wanabakije basi ungejiua wewe umuache huyo mumeo tunawatesa watoto hapo walipo hawaelewi watafanyaje tuwe na hofu ya Mungu kwa wote sio wanawake tu hata wanaume pia amekuchosha fukuzia mbali asije akakuletea balaa
Diwani hauko sawa , juzi mi nilichangia tu kuwa kama ameaamua kuwa na nyunmba ndogo abaki huko ,lakini we diwani kiongozi kabisa unahalalisha zinaa Kwa nguvu sana . ungekemea maovu yasiendelee ili watu wasiuane . hata na hivyo chui hali mnyama Jirani na makazi yake kama wanaume mkitaka kuwa huru na hamtaki kufuatiliwa na wake zenu angeenda Mwanza kuchepuka huko au mtwara aage kabisa ana safari ya kibiashara hata angeoa huko huyo mwanamke asingemfuata huko ,sasa wewe unapigia debe safari ya Toyo hujanibariki ingawa huyo mama ajafanya vizuri
Mshahara wa dhambi ni mauti hakunaga dhambi isiyo na malipo kikubwa hapo imeshatokea na huwezi jua amepitia mangapi na sidhani kama alikuwa na nia ya kumuua mune wake maskini
Diwani saidia jamii kwa kuwaelimisha,viongozi wa dini wapitie maswala ya vyeti vya ndoa vina vyowapa wananwake kiburi cha kumiliki wanaume, Imeshaeleweka hakuna monogamous marriages tuwe real
Yani uyu diwani jamani anaongea ovyo kabisa ndoa sio nyumba wala mali yoyote chamsingi nikwamba akufanya vema kuuwa mume ila usifananishe mali na ndoa alafu usiseme wanaume wataisha kemea mauwaji we vipi