Babu upo Sawa. Nawasihi wote tuyasahihishe yanayokera ktk mkataba huo ili Kwa pamoja tusonge mbele Kwa umoja wetu tuliorithi toka Kwa Waasisi wetu WA Taiga letu. insha'Allah tutaelewana.
Mwenye enzi Mungu amsema kwenye Qur Ani tukifu kwamba yaliyomo makafiri ni mazito zaidi kama nyinyi mutayaona. Basi hatuwashangai chuki zao zidi ya Waislamu. Mungu azidi atupe Uislamu ushindi. Amen.
Asante Sheikh Mohammed kwa kutujuvya na kutuzindua kumbe kuna madudu makubwa ya serikali ya Tanzania dhidi ya raia wake wasiokua “ WAKATOLIKI” inakuaje kuweka “ memorandum of understanding “ na Makanisa ya kuwasaidia mabilioni ya fedha ya walipakodi kwa Wakristo tu wakati wanasema serikali haina dini?
Hii ni njama YA Nyerere na inajulikana musiseme kua musiletewe udini baadhi yenu munao comment,, sisi zanzibar tumechoka na muungano hatuutaki kabisa ipo siku ishaallah Nyerere alitudhihirishia kua haipendi zanzibar haipendi uislam
Labda wee si Mkristo uanaehudhiria Kanisa. Waislamu wawazungumzia Wakristo nje ya Msikiti, ama Wakristo huwazungumzia Waislamu ndani ya Kanisa na nje yake. Kama hujui njoo tukuoneshe.
Mzee kila ulichokisema kinadhihilisha tatizo la udini ambalo waislamu mnataka kulileta ndani ya nchi. Mimi ni mkristo na maisha yangu yote miaka 56 marafiki zangu wengi ni waislamu na hatujakuwa na tatizo la kidini. Wakristo hatuna shida wala muda wa kuiongelea kuran au uislamu MARA nyingi nimeona ndugu zetu waislamu wakiwaongelea wakristo na kuongelea biblia. Wote tunajua kuwa dini ikiingizwa kwenye siasa ni HATARI KUBWA… ndio maana tukasema nchi yetu haina dini. Na serikali haihusiani kabisa na swala la kujenga shule au vyuo vya kidini hilo ni swala la taasisi, waumini, na dini husika. Swala la mkataba linahojiwa na watu wote waislamu na wakristo… wote hawapingi waarabu kuja kusaidia kuboresha utendaji na ufanisi wa Bandari zetu KINACHOHOJIWA ni baadhi ya vipengere vilivyomo ktk mkataba kuwa havina tija kwa Taifa. Mzee unaonyesha kuwa ulitaka Nyerere alete udini kisa alishirikiana na waislamu ktk Uhuru wetu… Nyerere hakuamini ktk kuendesha nchi ktk misingi ya kidini… kuwepo kwa wakristo wengi wenye Elimu ndani ya serikali wakati huo ilikuwa sio Nyerere alilileta bali lilitokana na wakristo wengi walikuwa na Elimu nzuri kutoka ktk shule za wamisionari. Tatizo waislamu wengi wakati huo walijikita sana ktk Elimu ya madrasa/dini. Ningesema mengi ila nadhani unapotosha umma na sio kitu kizuri… UNALETA UDINI KTK SWALA HALIHUSIANI KABISA NA DINI ZETU… madhara ya mkataba hayatajali dini ya mtu, yanaathari kubwa kwa wote waislamu/wakristo.
Huyu mzee sijamuelewa maana tunazungumzia kuwa kunavifungu vya mkataba wenyewe haupo sawa yaani kuna tatizo sasa yeye ndiyo kaleta zaidi mambo ya udini badala angesisitiza watu kuwa pamoja
Halafu huyu mzee anataka atuthibitishie kwamba Dini ya Ukristo ni ya ubaguzi wa rangi akidai kwamba Uislamu hauna ubaguzi wa rangi. Mbona sasa Waarabu walifanya Biashara ya Watumwa kwa Babu zetu kama hawana ubaguzi wa rangi? Wote Wazungu na Waarabu na watu weupe walitubagua na kututawala na hii wala haihusiani chochote na Dini. Kwanza hao DP World anaozungumzia watendaji wengi ni Wazungu na watu wa nje wala sio Waarabu kama anavyodhani. Kwani Mkataba wa DP World utakunufaisha nini wewe kama Mwislamu au Mkristo? Nimeishi Arabuni wengi hawana elimu bali wanatumia Wazungu na Wahindi kufanya kazi za Kitaalamu. Watu weusi wengi wanabaguliwa sana.
Daah huyu Mzee Mohamed Said pamoja na kuwa mwanahistoria mzuri sana, lakini huwa hawezi kuangalia jambo lolote bila kuvaa miwani ya dini. Kwa mfano, hili la bandari mbona halina udini wowote jamani?
Mzee kanishangaza sana hata Mimi. Kumbe nchi hii kuna watu wana UDINI hivi?? Mimi hata kwenye uchaguzi sijawahi fikiria dini ya mtu kabisaaaa! Nahisi sina wivu na dini yangu, inabidi niamke aisee.
sijui unaelewa au huwelewi au ndio unafanya makusudi. jifiche kwenye hiko kichaka lakini baadae utajutia ubinafsi wako. kwani hujui aliye wasema waislamu na wazanzibar badala ya kujadili mkataba? ikiwa Lema alikiri na kuonesha kuwa Samia ni rais wetu wote kwani hujui alikuwa anamaanisha nini. chokoeni tu nafasi ni yenu
Udini upo mbona hampingi mkataba wa MoU wa makanisa na serikali kama ninyi mna tetea maslahi ya nchi mbona hamkulalamikia jueni kuwa nchi hii si yenu kwanza mko wachache sana asilimia zaidi ya sitini ni waislamu tuheshimiane tusidhulumiane wala tusikwazane..!
hakuna mkataba wa bandari, hizo ni porojo za wapotashsji wasioitakia mema nchi hii. fatilia hutuba za waziri mkuu. na ndiyo maana hakuna yoyote anayeweza kuutoa huo mkataba hadharani na akaonesha mapungufu yake, wanachokifanya ni kuwahadaa watanzania kwa kutumia mkataba wa makubaliano ya ushirikiano wa kiinchi kati ya Tanzania na Dubai. Hao wapiga porojo wana ajenda ya siri kuwavuruga watanzania ili kuimarsha chama chao na hata kuzuia usimamizi mpya wa kampuni inayotajwa ambayo inaonekana wazi itazuia wezi wanaoiba hapo ambao asilimia kubwa ukichunguza utagundua ni watu wanaotoka ktk kanda inayowaunga mkono wapiga porojo hao, hao ni watu wao wanaonufaika na hiyo hali iliyokuwepo hapo na ndiyo maana hauwezi ukasikia wakiutaja ufisadi unaofanyika bandarini hapo zaidi wao kung'ang'ana na upotoshaji huku wasiojua kuna mchezo gani unaofanyika wanabaki kuwa wasindikizaji kwa kufata mkumbo wakihisi wanasapoti uzalendo kumbe na wao wanasaidia harakati za kuwabakisha wezi bandarini.
Huyu mzee huwa ana udini sana, kila akifungua mdomo lazima alete Ukristo na Uislamu, hizi dini tumeletewa tu jamani sisi sote ni watanzania, tujadili kwa mantiki ya utanzania wetu
Mkuu umeongea vizuri lakini hata aliyekuwepo Bandarini Nazri Karamagi ni Muislam. Hapa sio udini tusiendekeze hayo. Hapa ni vipengere vya Mkataba ndo vijadiliwe, lakini pia Kumtaja Rais kusiwepo kwa sababu ahusiki na Makando kando haya. Yeye alimpa Jukumu msaidizi wake (Waziri) naye ana wasaidizi wake Wanasheria ambao nadhani ndo walizembea kupitia Mkataba ule. Naona mambo yanazungumzika na yanajadilika . Tuwe watulivu na tuzungumze wala hatuhutaji kuhesabu Waislam ni wangapi na Wakristo ni wangapi, hebu tutazame Utanzania kwanza.
Kikweli watanzani hawajazungumzia dini. Watu wanazungumzia masharti mabovu ya mkataba. Ninyi mnapata wapi hahari ya dini?. Waislam tusipoacha mambo ya kuzuazua basi sisi ndio tutaanzisha mambo ya udini ndani ya tanzania. MASHEHE ZETU ACHENI MAMBO HAYO!!!!!.
Sahihi kabisa..kama ni waarabu kuwekeza wapo mbugani tokea mwaka 92, kujengwa bwawa la Nyerere lipo chini ya Misri..mara hii jibu kwa hoja mkataba una mapungufu au hauna sio unasema Tu udini
Kwa hiyo huu ukweli anaouzungumza ww uliwahi kumsikia Nyerere anasema? Kwani si kulikuwa na jumuiya ya Kiislaam kiongozi wake Sheikh Swaleh Bin Ameir Nyerere kwa kuona maendeleo mazuri kwa Uislaam akaivunja? Na Mali za wa Islaam kutaifishwa? Sasa ww hoja yako nn kutuhumu Waislaam? Fuatilia historia vizuri.
Mohames Saidi yeye kila siku kuhubiri udini tu Badala ya kujadili mkataba na vipengele vyake vyenye utata mnadjili dini na ukabila mnacheza ngoma ya CCM
Mazungumzo haya yamiasha hisia za wengi waliosikia na watakao sikia ninawaomba tuwe makini kunapojadili tuvumiliane hizi chokochoko za udini ni hatari kwa usalama wa taifa siyo jambo la kufanyia ushabiki. Na viongozi wetu waache kutumia udini kama silaha. Wakemee mjadala wa kidini. Tunafanya uchanguzi tangu uhuru kiongozi huchanguliwa na waislamu na wakristo hakuna udini. Wote bila kujali dini tukutane kwenye masilahi ya taifa Kwa vizazi vijavyo. Dini isitufanye tuwe wajinga.
Udini unakuja wanapo jadili masuala haya waislamu tu Kaka?? Mbona askofu mwakipesile anaongea mazito juu ya udin hasa uislam na hakuna and dauti acha udini we nakujiona wakiristo mupo swa mapuwa ww
Wakiristo Siku zote wanajizima data Wao Wakijadili Maslahi ya Kitaifa kidini dini wanaona sio Udini ila kwa wengine ndio unazuka Udini Nashindwa Kuelewa
Waislamu tatizo lenu ni uongo. Katibu mkuu wa baraza la mitihani la taifa ni muislamu. Nini kimebadilika? Halafu wewe mzee mbona tunawalaumu wazungu kwa ubeberu? Huyu mzee anafikiri DP Wotld ni ya waislamu, anafikiri inakuja kujenga misikiti au itakuwa inagawa pesa na ajira kwa waislamu. Hiyo ni kampuni ya watu wenye hisa toka mataifa na dini mbali mbali. Lengo lao ni kupata faida ya pesa na siyo kueneza dini. Ni mzee asiye na busara hata kidogoo. Yaani kuikataa DP World ni kukataa waislamu? Na watu wanachopinga, ni vipengee vya mkataba. Anavyoongea, utafikiri ni mwarabu. Pambafu kweli na mwongo mkubwa.
Nyerere alipokua anapiga kelele za udini alimasnisha waislam Wakae kimya hata wakifanywa chochote tatizo hamumjui kwasababu kauweka ugalatia juu akaukanyaga uislam uliomueka juu someni vitabu vyake alivyotunga mwenyewe au kile cha (jimbo kuu la daresalam) mwenyewe amesema nilazima kanisa aliweke juu wakati akimjibu pedre John sivalon wakati alipo muuliza utalifanyia nini kanisa?! Nakweli katudhalilisha sana waislam wenyewe tunajua! Nahata viongozi wakubwa wamekua wakitamka wazi hadharani wakionesha chuki zao juu ya uislam akiwemo Lukuvi tena akiwa kanisani !! Kama hamjui chuo kikuu cha Dar ni cha waislam muhimbili ya waislam mpaka ikulu ya Dar ilikua chuo cha Kil Islam sema wengi hawajui ila ipo siku haki itakaa juu kama sio sisi basi wajao wataiweka hakii juu !!!
Chokochoko za kumfanya Nyerere alikuwa kitu kidogo hàziwezi kutusaidia chochote maana ni wazi kwamba alikuwa na marafiki na maadui vile vile. Namuona Mwandishi akijenga hoja ya kuuinua udini zaidi kuliko hoja iliyopo ambayo wengi wanajaribu kuitumia zaidi kuitetea DP World.
@@gessanabuu2099 Tatizo ni matumizi ya akili tu... maana kuna watu wanajifanya waislamu kuliko hata Mtume Muhammad (S. A. W). Kuna haja gani ya kulazimisha tujadili uislam katika mkataba wa DP world. Bahati mbaya kila waislamu wengi wanadhani kila anayeutaja uislamu basi anautetea kumbe wengi wanajificha tu katika uislam kutafuta huruma ya waislam baada ya kutuibia au kutumika na mabepari kama kondomu.
Achani kufikiri kua waislam watafaidi ikiwa bandali yetu watgawiwa waarabu bure kinacho daiwa ni mkataba mbovu ambao unagawa mali ya nchi bure kwa waarabu wa dubai
MGOGORO WA BANDARI TATIZO LAKE NI VIFUNGU VIBOVU VILIVYOMO NA SIYO TOFAUTI ZA KII AMANI. UELEWE VEMA JAMANI. KUNA WAISLAM WALIO UELEWA MKATABA NAO WANAUPINGA.
Ni mwalimu mzuri wa historia. But hapa ni ishu seriously haitubadilishi mindset. Hapa ni msimamo wangu binfsi sipependi MUUNGANO. Naburuzwa jamani hee!!
Sioni Logic ya haya maongezi, ninachoona ni wazanzibari wawili wanajadili mambo ya Tanganyika tuu.. kama wadubai wazuri wapeni bandari yenu huko Zanzibar.. na huu muungano Bora ufe.. badala ya kujadili maisha nyie mnajadili dini
Jaman me naamini kunawaisilamu wasomi sana nyie haumuoni mkataba ni mbovu ,mkataba gani hauvunjiki,, mkataba gani hauna consideration ,mkataba gani hauna time,,,, tusilete udini na uzanzibar na ubara ,, dibouti wanalia adi Leo na mkataba wa DP world kwani dijibouti ni nchi ya kikristu
Hivi kujadili huu Mkataba na kuupinga inahusiana vipi na Uislamu au Ukristo? Ninyi ndio mnaoleta Udini sasa. Yaani hata kama Mkataba una utata mnataka watu waukubali tu kisa eti umeletwa na Waarabu? Kwani mnadhani DP World wanafanya kazi Waislamu peke yake? Acheni Udini jadilini maslahi mapana ya Nchi. Mimi ni Mwislamu na naukubali sana uwekezaji lakini huu Mkataba ni muhimu sana ujadiliwe
Kwa hiyo haya yote mkataba wa namna hii umeletwa na udini maana mimi siamini kuwa katka udini naona kuwa viongozi wetu wawe wapole waache mihemuko maana wananchi wanauliza vifungu vya mkataba ambao unaonyesha kuwa mkataba unatatizo kumbe kuna mambo ya siri
Changamoto inabaki kuwa muda ushapita na watu washachukua mkondo mwengine kabisa wa historia ya nchi hii. Hata mambo kama haya ni kama paukwa tu na Shekh anaonekana kama mtu anayezusha tu khabari hizo. Wapo waliotaka tufike hapa, na huenda hata huyo Nyerere akifufuka leo atapinga kila kitu [ tujadili na mashinikizo ya Makoloni yalikuwepo tangu ]. Kilichobaki sio kuzungumza juu ya makosa ya wakristo wala kudhulumiwa kwa waislamu ila kuliunganisha taifa pamoja .Mimi nawaza hivi habari hizi wakristo wanapozisikia watachukua mkondo gani angali nao mamboa wameyakuta tu? MTU ASIYEJUA HISTORIA YAKE AKIVUTWA HUKU ANAKWENDA , AKIVUTWA KULE ANAKWENDA
Labda nikuambie kitu kadinari pengo anayafaham haya na wengi katika wakristo walio na nyadhifa kukwa wanayajua haya , sheikh kajaribu kuwarejesha watanzania katika ummoja kwani wamesikika viongozi kadha wa kisiasa kama mboe akisema suala la udini na ukabila akifingamanisha na DP WORLD, nawakati yeye alitakiwa kuzungumza mkataba tuu , sio mafungamano ya udini na ukabila nawakati watu wanajua historia kubwa jinsi waislam walivyo pambania uhuru
Kwa hakika ndugu Mohamed ameongea kwa hisia kali lakini kwa uungwana. Ebu wahusika kwa Nia njema waujadili mkataba ibara kwa ibara bila kileta yale ya Nje Mkataba- Uislamu, Uzanzibar nk. Watu wazima tena wasomi Watanzania wanastahili kuwa na akiba ya maneo, kuwa wakweli na warejee katika dhamira yao ya ndani kabisa.
Mohamed saidi si mdini kama mayo coment!!ila siku zote ukiongelea kuhusu uislam u,utaitwa mdini!!l Maana maana ya udini kwa tsfsiri ni kuutaja UISLAM!!
wakiristo walikuwa hawana haja ya kugombana na wazungu wakoloni,maana wazungu walikuwa wakiwapa watu wa makanisa good chase!na kanisa likisaidiana na wazungu ktk kutawala!!!
Hutumpingi Mwarabu wala Hatuwakatai Waarabu Na Dini sio ya Mwarabu Bali DINI ni ya Mwenyezi MUNGU Wote Tunaipenda sana Tunacho hoji ni Mkataba wenyewe ndio maana wenye Akili wote Wana hoji Pr Lipumba/ shiviji pia wana hoji Tusichonganishwe
Huna la kutuambia watanzania, huko nyuma ni ya wakati huo, watu wameamka huwezi kutuambia tugawe rasilimali za nchi kisa kiongozi kaamua. Nenda wanaojua kusoma mkataba, acha mambo ya udini, hivi dini itatusaidia nini na kizazi kijacho?
Hakuna udini ninachoona hapa marumbano wenzetu wanaojua sheria wanasema mkataba ni mbovu kwani bala hakuna waislamu watanzania wote bala na visiwani tuwe makini kwenye suala hili la bandali ili wanasiasa wasitugawe kwa propaganda wanazoleta kuingiza udini kwenye ishu inayohusu maisha yetu na vizazi vyetu kama watanzania nilichoona mbinu nyingi ovu zinatumika na wanasiasa wasiopenda muungano wetu kwa kujalibu kuingiza suala la bandali na udini tuwe waangalifu na tuache kutumiwa
Bwana Ibin Saidi kuna mambo unachanganya vibaya hivyo akiwa mwislaam atuibie tu akitujengea miskiti inatosha? Hapana hivyo unasema mkataba hauna dosari?
Sheria na nguvu za kuitawala Tanzania ilitengenezwa toka baada ya uhuru na serikali ya mwanzo ya Nyerere,iliyolipa nguvu kanisa,kuingia mkataba kama wa MOA,wa kuliaaidia kanisa kwa pesa za walipa kodi,leo ubalozi wa Vaticani upo Dar,waislamu wanazuuliwa hata kujiunga na jumuiya ya kimataifa ya kiislamu,OIC,mkataba wa bandari mwezi huu wa Zanzibar chini ya ufaransa/wazungu/wagalatia/wakristo hujasikia pingamizi,kwa kuwa kama ulivyosema mkataba wa Dar chini ya Dubai/waarabu/waislamu,ndio imekuwa shida???,kuwa na imani hii sio haki.
Shekhe hapa tunashauriana habari ya mkataba sio dini jamani hiyo history mbona unaisumulia mara nyingi kwasasa tunaongelea mkataba wa DP world 🌎 sio dini msitake watu kuanzisha vitu vingine please tuko na mkataba!!!!
Serikali ishatoa maelekezo ya kutosha. Haya ni maridhiano mkataba bado. Ila choko2 haziishi, tuache chuki jamani. Tusiangalie muwekezaji kwa dini zao tuangalie uwezo. Karibu mdubai
Unaelewa nini ww kaa kimya subiri kufa tuache vijana wetu wakuwe nyinyi ndiyo mliwabeba mabwana watu kibao na mnambeba bwana mmoja mnakuuzwa mtu mmoja anawauza
Emotions apart, " vyombo husika" using sober professional cadres wazungumze na huyu Ustaadh kwa nia njema ya kujenga Mama Tz..na kisha kuishauri Govt..waache vitisho..These are issues C za KUPUUZA!!😮😮
Ma ustadhi mdichanganye mambo hakuna anaelataa DP world kinachokataliwa ni mkataba shehel hapo kuna wahuni wanapiga upatu sio lingine ndugu zangu kwa upande wangu ninavuoelewa !!!!!
Jamani kinachochanganya watu ni mkataba na sio uislamu wala.ukristo hata angekuja mkristo kama mkataba haipo wazi lazima ingeleta shida sasa mbona mnalazimisha kuongelea udini???
Hivi wahariri wrote wa magazeti yaliyomshambulia Mwinyi walikuwa waisiliamu? Jamani tuwe wakweli . Hivi serikali sasa na bunge ni vya wakiristo tu.Wewe mzee ndiyo unaanzisha matatizo ya ubaguzi. Kwa nini ufikirie kujengewa misikiti na DP World.
Je uhuru uliokusudiwa na Skyse na wazee wengine ulikuwa kwa ajili ya Dini ya Kiisilamu? Je hayo yasingewatokea waisilamu yasingewatokea wakristo? Mchungaji Mtikila alimpinga sana Nyerere, Mtei alipishana na Nyerere, Tundulisu alimpinga sana JPM lakini hawa wote ni Wakristo... Kwa nini Raisi akiwa muisilamu akipingwa mnasema anapingwa dini yake?
@juliuskitaluka1206.Kama "watu wanaongea udini ni watu walioishiwa maarifa" ni yepi? 1) Udini wa Ukiristo 2) Udini wa Uislam 3) Udini wa Upagani Mkatoliki Nyerere alianzisha Udini kabla ya Muungano, seuze Waziri William Lukuvi Kanisani. Lakini kwa nini wote hawakulaumiwa? Ujamaa wa Nyerere ulikuwa wa Udini wa Kikatoliki. Aliwalazimisha Waislam kufuata Udini wa Upagani.
Mkoloni tuliyemuondoa hapa Tanzania alikuwa mkristo na Nyerere sialikuwa mkristo mbona tumfukuza wingereza ambaye ni mkristo ....waarabu ni waslamu ni kweli lakini sisi tunatetea bandari zetu kwakuwa mkataba ni mbovu si dini hapa...tunapotetea chetu hatuna cha uislamu au ukristo tuna utanganyika....sasa mmejisahau mnaleta udini ...Ok mnacheza na moto
Sahau Tanzania hakuna dini familia tumeungana mpaka kufikia baba muisilamu watoto wakristo mama hana dini hujawahi kuona familia kama hizi hapa tanganyika labda zanzibar hakuna lakini hapa tuko wengi
kama ni waarabu kuwekeza wapo mbugani tokea mwaka 92, wapo Serengeti mlisikia watu wakikemea kwa nguvu hivi? kujengwa bwawa la Nyerere lipo chini ya Misri..mara hii jibu kwa hoja mkataba una mapungufu au hauna sio unasema Tu udini
HAO WANAO PAMBANA KUKITOA KIFUNGU HEWA KWENYE MKATABA BAINA YA DUBAI NA TANZANIA. BASI NAO WAKUMBUSHWE ULE MKATABA WA MAKANISA NA SERIKALI YA TANZANIA MWAKA 1992