Mtoto akizaliwa vizuri, na akakua vizuri, na akawa kwenye mazingira ya kazi anazozipenda ni zaidi ya phd. Ubongo tulionao ni sawa na mtu yoyote yule duniani. Mfumo wa elimu ya Tanzania ni mbovu sana, Unachofanya ni kuharibu miaka ya watu. Ingetakiwa elimu iwe kwa vitendo. Na sio mtu anasoma theory mpaka anakuwa mzee. Akikutana na kitu halisi hawezi chochote na vyeti vyake vyote.
Mtalaumu wakoloni mpaka lini? Wakati ni ujinga wenu waTZ? Mnabeba madafyari 12 ukimaliza form4 huwezi hata kulinda Kwa geti Kwa mzungu, huwezi hata kuendesha pikipiki, huu ujinga mkoloni kafanyaje? Mnala,imeisha lugha ya kufundishia wakati Katiba yenu na Sheria pia kanuni mnatungiwa kiingereza, mkoloni kaharibu Nini? Wanakuja wawekezaji wanasema bizaa zao zinafaida kubwa hivyo Bei ishuke Ili watu wengi wanunue mnasema Kuna Bei elekezi, hapa mkoloni kaharibu Nini? Msiposimama kuibadilisha wenyewe TZ yenu hakuna mtu atawabadilishia. Mitaala ya elimu ni mibovu inatoa wanafunzi vilaza. Mtu anamaliza Form6 Hana lolote ambalo kama ataidhia hapo anaweza kufanya Kwa alichokisomea zaidi ya kusoma na kuandika,,, yaani anaingia chuo ndiyo anachagua asome Course gani! Na anamaliza chuo anaenda kuwa mwanafunzi Tena wa Course aliyosomea apate uzoefu. Msimlaumu mkoloni akili yenu imelala sana.
Wako wapi hawa watu? Kwa nini hamuwasaidii kuanzisha viwanda? kwani kuna tofauti gani ya trekta na gari hizi na vile tunaagiza nje? Waafrika tuanze kujiamini sasa,tuanze kuwaamini watu wetu,tuwawezeshe ndipo tutakuwa huru na kuheshimika duniani!
Unahitaji kumfahamu uyu jamaa mi nimekutana naye Ana kwa Ana Tatizo nikikupa namba yake itakuwa sio POA chakufanya Ni kumtaftia Ela ya smartphone ili aje store namba zake