DAR ES SALAAM: RAIS Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.
Utenguzi wa Waziri wa Habari umekuja siku chache baada ya wachambuzi wa siasa na watetezi wa demokrasia kumnyoshea kidole Nape Nnauye kufuatia kauli ya “utani” aliyoitoa wakati wa ziara huko Bukoba mkoani Kagera.
Wakati sababu za kumuondoa January Makamba katika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Nje hazijafahamika, Rais Samia amemteua Balozi wa Tanzania nchini Italia, Balozi Mahmoud Thabiti Kombo kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje.
Katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk. Moses Kusiluka Rais Samia amemteua Jerry Silaa kuwa Waziri wa Habari, Mawasialiano na Teknolojia ya Habari. Silaa alikuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nafasi hiyo itaongozwa na Deogratius John Ndejembi aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu).
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: ....
SpotiLeo: ....
TWITTER;
Twitter HabariLeo: Ha...
15 сен 2024