Тёмный

Salama Na WALTER CHILAMBO SE6 EP59 | HABA NA HABA PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460 

YahStoneTown
Подписаться 395 тыс.
Просмотров 16 тыс.
50% 1

#SalamaNa #SendTip MPESA #5578460
Pengine jina la episode hii linaweza likakupa muangaza kidogo wa story fupi ya maisha ya mgeni wetu wa wiki hii kwenye kiti chetu chakavu na meza ya kigae ambaye leo hii tayari kashaona, tochi ya maisha kwake inamulika tu vizuri na mbele anapaona. Huyu ni Walter Chilambo ambaye miaka tuseme 14 iliyopita alikua hana uhakika wa chakula chake cha siku tu achana na sehemu gani atalala. Ruka ruka ya kule na huku na bahati ya kupendwa alonayo na ambayo inaendelea mpaka leo naamini inakuja kwasababu ya ukarimu wake na hii ndo silaha yake yenye makali ambayo inampeleka mbali mpaka leo hii
Kama mtoto wa kiume ambaye unatakiwa kwenda kujitafuta ki maisha Walter nae ilibidi afanye yale yale ambayo si watoto wa kiume tu ila wengi wetu tumefanya ya kutaka kwenda kutafuta chako, na yeye aliona basi bora afanye hivyo. Safari ya kuja town kutoka mkoani anatuhadithia kwa upana kwenye episode hii. Mtu ambaye alimpokea ni mwana tu ambaye alienda nae shule moja, stop ya kwanza? Keko Magurumbasi. Na si kwamba alikua hana Ndugu hapa Dar es Salaam yeye alijiamulia isiwe hivyo, ilikua ngumu kumshashiwi Mama yake ambaye alitaka kujua ramani nzima ya mwanae ambaye alikua anakuja mjini kwa mara ya kwanza. Baada ya kufanikiwa kushawishi Mama Walter, kijana alipewa nauli na ananiambia by the time anafika Dar alikua na shilingi ELFU MOJA TU kwenye mfuko wake, hapo ni Ubungo kwenye stendi ya mkoa
Imani yake kwa Mungu wake pia ni silaha ya pili ya Ndugu Walter Chilambo. Hii ndo ambayo kwa mujibu wake imemsaidia kumvusha na mengi, maisha huko Keko hayakua mazuri, sikutaka kutumia neno si kama alivyo yatarajia maana hata yeye hakua na matarajio yoyote kwasababu alikua hajui anakutana na mazingira gani wakati anaenda kwa mwanae huyu aliyesoma nae Sekondari ambaye walikua na majina ya Baba yanayofanana. Mwenzetu anaitwa Michael. Alikaa pale huku akiwa anajaribu kuji tafuta ila kila anachogusa kilikua cha moto. Ananihadithia jinsi alivyoanza kufanya kazi za kila siku ili angalau apate hela ya kula, kule kwa Mama alikua anajifanya kama kila kitu kinaenda vizuri kwahiyo hata vimzinga vidogo vidogo vilikua haviendi. Ulipofika wakati wa yeye na mwanae Michael kufunguana mashati maana alikua ashakaa saana na hana dira nzuri hapo sasa ndo kila kitu kilianzia.
Unadhani mmoja anaweza kuwa na bahati kiasi gani kwamba mtu ambaye aliombwa amhifadhi kwenye ghetto lake wakati yeye anatafuta ustaarabu mwengine kuwa ni Ndugu yake? Pengine hii hutokea kwa wenye BAHATI TU, pengine Walter ni mmoja ya watu hao maana baada ya kujulikana hilo ndo angalau kukawa na ahueni ya kuwa na uhakika wa sehemu ya kuegesha mbavu, hii ni moja ya sehemu ilonisisimua kwenye simulizi yake, imagine mtu anavyokua kapigika alafu kutoka ambako hakujulikani mtu ambaye ameombwa akuhifadhi kwa muda anatokea kuwa ni Ndugu yako, hii ni Mwenyezi Mungu pekee ndo ambaye anaweza KUTENDA na kama utakua ushawahi kuishi kama ndege ambaye hajui analala wapi basi wewe utaweza kuelewa zaidi hapa.
Walter Chilambo ni mshindi wa Bongo Star Search wa mwaka 2012 na baada ya kushinda alianza safari yake ya muziki rasmi. Safari yake haikua ya urahisi kama ambavyo naamini alitarajia au sote tulidhani. Kiwanda cha Bongo Flava ki usalama tunaweza kusema kina wenyewe na ukiwa mpya kabla hujajua fagio lipi ndo linafaa kusafishia wapi basi kazi utakua nayo. Kwa Bwana Chilambo ambaye alishinda taji na pesa hakukua na tofauti kabisa. Neema kwa upande wake ilianza kuonekana baada ya yeye kuamua kufanya mziki wa kumtukuza Mungu na baada ya hapo mengine ni story tu.
Kwahiyo NINI hasa kilimfanya afanye maamuzi hayo? Kwenye kipindi ambacho kila mmoja ameamua kuimba nyimbo za mambo ya kitandani na mambo ya ndani je yeye kwanini aliamua kubadilisha gea? Maana Kama sauti anayo na kuandika anajua sasa sababu ni nini? Na pia wasiwasi wangu uko kwenye baada ya ‘kutoboa’ huko aliko na kupata umaarufu na sifa tele hatorudi tena huku kwenye kuimba nyimbo za kuachwa na kupendwa na kutendwa? Ana uhakika kiasi gani? Ukichukulia kama kuyaona na kuyafanya basi ashafanya mengi?
Nataka nikuachie hapa kwa leo ili uweze kwenda kuskiliza na kuya enjoy maongezi haya na mwanangu huyu ambaye hajabadilika, bado mcheshi, mwenye heshima na anayejitambua. Natumai hadithi yake itaku inspire kwa vile ambavyo ningependa iwe.
Amina.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪RU-vid Link bit.ly/RU-vidSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Развлечения

Опубликовано:

 

19 мар 2023

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 35   
@imasigaro2968
@imasigaro2968 Год назад
Maisha yakukua bila upendo wa baba zetu yanatugusa wengi ,Mungu awabariki wakina mama wote dunia ,endless love from them ❤️
@kitwanathabiti
@kitwanathabiti Год назад
@cheka480
@cheka480 Год назад
@candymercious8268
@candymercious8268 Год назад
Amen
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 Год назад
Salama sitakaa niisahau cku uliyomwambia Walter kwamba ungekuwa na uwezo ungemtia mfukoni watu wakakutunza hela ♥️daaah long time.
@newtonmnyack9729
@newtonmnyack9729 Год назад
Nakukubali Sana mdogo wangu ila nilifurahi Sana kwa Mara ya kwanza nisikia ukiimba Asante kwa ajili ya kumshukuru MUNGU nikaona hapo ndio mahali sahihi MUNGU akubariki Sana kwa Hilo nakutakia mafanikio mema. #andazi maji ya kandolo,.
@zebedayomshani
@zebedayomshani Год назад
Watu wa mungu ni wa kweri mno hongera brother 💪
@Heavyweight1111
@Heavyweight1111 Год назад
Wa5 leo Nipeni like zangu
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 Год назад
""Umenitoa mbaali kusikojulikanaa"""I loooove this"kama wewe ulifuatilia BSS ya Walter utaelewa maana ya huo mstari wa huo wimbo hapo mwanzo"meeeen these 2🤣🤣🤣🤣
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 Год назад
Preach Walter preach""we forgive for our own healing n not for their wrong doing.
@Bob-kz2ql
@Bob-kz2ql Год назад
😅😅😅Salama never stop to amuse us na intro zake asee this is powerfull…Walter keep going,kuimba gospel inataka moyo in terms of payment shows nn ila uko vizuri God bless you mpendwa
@rehemaothman2475
@rehemaothman2475 Год назад
Ameen
@elia5475
@elia5475 3 месяца назад
Ubarikiwe sana blaza
@doreen9516
@doreen9516 Год назад
Ubarikiwe sana Walter! 🙏🏾
@namelockmaasailady8002
@namelockmaasailady8002 Год назад
I love you my lovely sisy salama💞💞💞you are doing great.
@mountaincoffee7
@mountaincoffee7 Год назад
Golden voice
@marrymchaki9025
@marrymchaki9025 Год назад
Nani anakikubali salama ....anipe like zangu apa
@ArexIsack-ex9pt
@ArexIsack-ex9pt 9 месяцев назад
God bless you salama
@lowkeybongo
@lowkeybongo Год назад
Bomang’ombe ❤️🔥
@musambaruku6661
@musambaruku6661 Год назад
Salama Na ❤❤❤
@isayamandevu833
@isayamandevu833 Год назад
Aisee mimi ni shabiki yako, napenda namna unavoeka page zako za mitandao ya kijamii kwa upekee , na napenda mengi ambayo mengi SIWEZ sema APA But ninakuomba umlete na pastor Myamba
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
🙌🏿
@ibrahimzuberi1029
@ibrahimzuberi1029 Год назад
Wakwanza
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
🙄🙄😳😲😲😲2019 au nime sikia vibaya??????????
@monicajohn2515
@monicajohn2515 Год назад
Naona alitaka kusema 2009
@emmanuelywambura2006
@emmanuelywambura2006 Год назад
Mshikaji wake na reivani wanatoka mtahaaaa mmoja na Mimi ndio mtu wa kwanza kurekodi kazi zao dar most record pumbavu
@emmanuelywambura2006
@emmanuelywambura2006 Год назад
Pumbavu namjuwa huyooooo muongoooo mpumbavu Sana uyu dad's salama sio mlokole no Kiki mpumbavu Sana namjuwa mungu wangu Mimi namjuwa toka anamiaka 0
@josephk90
@josephk90 Год назад
Alikukosea nini mkuu mbona unamchukia mno?
@luogafrank3205
@luogafrank3205 Год назад
Jamaa kashaokoko na demu wako alikuachia mbona kitambo tu move on jamaa
@emmanuelywambura2006
@emmanuelywambura2006 Год назад
Pumbavu namjuwa huyooooo muongoooo mpumbavu Sana uyu dad's salama sio mlokole no Kiki mpumbavu Sana namjuwa mungu wangu Mimi namjuwa toka anamiaka 0
@veronikabaraka3315
@veronikabaraka3315 Год назад
Nan muongo Sasa hapo
@mariajoseph9735
@mariajoseph9735 Год назад
Si ameshakwambia aliamua kubadili mwenendo wa maisha yake
@miriamumbwilo164
@miriamumbwilo164 Год назад
Annoying comment🚮😏😏 Et sio mlokole bro..are you God? Who are you to judge...eniwei akili🤌
@liducakes2803
@liducakes2803 Год назад
​@@miriamumbwilo164 100%
@luogafrank3205
@luogafrank3205 Год назад
Namjua huyu jamaa kabda ajaokoka alimchukua demu wa emanuely wambura lakin sasa hivi kaokoko
Далее
Камень, ножницы, нейронка
00:33
Просмотров 64 тыс.
Salama Na Shikana Ep 17 | DYNAMITE Part 1
29:48
Просмотров 338 тыс.
Walter Chilambo-Sijawahi Ona (official Video Lyrics)
3:50
This or That 🛍️
0:52
Просмотров 6 млн
Да блин 😀
0:19
Просмотров 1,5 млн