Waswahili husema kazi ni kazi bora mkono uende kinywani, lakini je umeshawahi kuwaza kazi ya kunyonyoa na kusafisha vichwa, mikia, ulimi na hata miguu ya ng’ombe na mbuzi kuwa ni kazi ambayo endapo utajitosa unaweza kuvuna pesa.
Kama hufahamu kutana na vijana watano waliojiunga na kufanya kazi hiyo kando ya machinjio ya Kizota Dodoma ambao huvuna kati ya shilingi 80,000 hadi 100,000 kwa siku wakinyonyoa na kusafisha viungo hivyo kutoka kwa wafanyabiashara wa supu wa maeneo mbalimbali ya jiji la Dodoma.
✍@official_jennifersumi
#azamnewsupdates
29 авг 2024