Wamarekani sio watu wa kuwaamini hapo asaivi wanamuita Will Smith bwege lakini akisema ajibu mashambulizi pia wata mgeuka na kusema mnyanyasaji wa wanawake
Daa pole will Smith,,will Smith Bado hajamuv on hajampata mbadala wa Jada..Yan mim ilinikutaga hayo kumpenda mtu kias icho Cha will..ni hali mbaya Sana ikikukuta..nikwer will ni king'ang'anizi Kwa Jada na upendo upo upande mmoja..pole will mungu atakutoa huko
Yan mapenzi yanaumiza Sana na mapenzi ni uwendawazimu unaweza ukaitwa majina yote kabisa lakin ogopa Sana kitu kinachoitwa kupenda ,,kupenda jaman nikitu kibaya Sana,,,hususan kama hujamuv on kwamtu unayempenda mmmh nihatar..unaweza hata kujizuru..Mimi nakuelewa Sana will Smith..inavyonekana Jada alikuwa hampendi will Smith tokea awali..ila aliolewa tu na Smith ilimladi tu aolewe
Mwanaume kuoa Marekani ni sawa na kujitega mwenyewe mda wowote unanasa... Huko utaishi vizuri ukiwa bachelor ila ukioa maisha yako yatakuwa na misukosuko mwanamke hachelewi kukugeuka au kuomba talaka mgawane mali.
Yaani wenzetu hawa Hawatuthamini kama ss ni binadamu kama wao weupe. Uchafu wote tunatupiwa watu weusi. Mashoga sisi mashetani sisi, kila baya ni la ss weusi. Ukipata umaarufu hawapendi watakusingizia kila chafu. Tujuwe hstupendi hata ukijikomba vipi hawatuthamini
kwakwel mapenz uchiz, jada alivyokuwa mbovu ivyo ata mvuto hana lakin mwamba anakomaa nae kwa machungu yote, Will Smith ni handsome boy sana nilimuona live arusha mwaka juzi aisee mwamba kapanda hewan na handsome anaweza pata pisi kali ingine akala nayo raha ila yeye kukomaa na uyo bibi tu
Sahihisho. Moja: tafadhali sana zingatia kuwa huku Tz hatuna shule za "upili" kama unavyoziita. Tunaita (na wewe unajua hilo) kuwa tunaziita shule za sekondari. Pili: Will na Jada hawajawahi " kuachana" bali walitengana kwa muda. Kuna tofauti hapo. Kwa Kiingereza ni "divorce au kuvunja ndoa" na "separation" au kutengana wakati bado ndoa ipo hai
Asikwambie mtu hakuna mzazi anayependa uhusiano wa mwanae wa jinsia moja,hata wao hiwaumiza ila baadae husema kama ana furaha yy basi ila hiwaumiza sana.