Nitaingia MBINGUNI kwa kishindo, hata Dunia nzima irudinyuma mimi siwezi...nampenda YESU KRISTO PEKEE ndani ya moyo wangu....kisu kipite shingoni, lakini MBINGUNI niingie...Dhambi ndiyo kizuizi cha Mwanadamu kwenda mbinguni, kuwa mtakatifu sana mpendwa ...1petro 1:15-16, waebrania 12:14...
Ukweli ni huu amini nawambia saut aitojirudia tena masikioni mwako usiposikia ujumbe huu ukaufanyia kazi utalia na kusaga meno, emen mungu akutie nguv mtumishi
Mchungaji Mungu akubariki sana sana unasaidia kuukomboa ulimwengu, watu tunapotoshwa na watumishi wa uongo paka tunakosa tumaini kabisa ila wewe ndie mtumishi wa Mungu wa kweli, unaesema ukweli na kufichua Siri nzito zilizifichika za manabii wa uongo nakupenda sana mtumishi na naikubali sana kazi Yako Mungu akuzidishie Maisha marefu yaliyojaa neema nyingi Ili uzidi kuikomboa Dunia 🙏🙏🙏
Amina mtumishi wa Mungu, unayoyafundisha yanaendana kabisa na anayofundisha mtumishi wa Mungu mwakasege, mfano kuna lile somo la....(mpe Mungu moyo wako auandae kwa yanayokuja)...Mwenye sikio na asikie,Mungu atusaidie,,Wa Kristo wenzangu tuamke
Mungu aturehemu sana. Tayari inaendelea na iko wasi ni Mungu atutie nguvu watakatifu wote duniani tusimame katika kweli yake tusimuasi Mungu. Yote aliyotabiri Bwana Yesu yametimia. Mungu awe pamoja nawe mtumishi kwa kazi hii nzuri.
Mungu akutunze Mtumishi..nakufuatilia sn, mafundisho Yako,tunaomba Mungu akuwezeshe utuandalie Somo la Jinsi ya kulishinda Hilo pambano,tufanye nini kama wakristo,na ikitokea tangazo la dini Moja,tupo makanisani, tufanye nini?tutaabudu wap? tunaomba utuandalie Jinsi ya kulishinda Hilo pambano la mwisho. SoMo la la tangazo la kifo kwa Wacha Mungu limenifungua macho,kweli inaogopesha Mungu tusaidie tu
Neema ya mungu iwe juuyako mtumishi wa mungu tupo vijana wenye kutamani kuujuwa ukweli mungu akupandishe viwango nasi tupate kuelewa zaidi k.t.k jina la yesu
Ndio maana ninapoona wakristo wamejazana kwenye mikutano ya kina Mwamposa ninalia kwamba njaa ya neno ni kubwa sana. Watu wanafuata udanganyifu wa miujuza, njia ya upotevu ni pana na ni wengi waipitayo njia ya mbinguni ni nyembamba waipitao ni wachache
Ubarikiwe mtumishi kwa kweli hizi ipo vita ya ibaada nani aabudiwe kati ya Mungu na. Shetani Tunakoelekea na harakati zishaanza ni kwamba jumapili inaenda kutangazwa kuwa siku maalum ya ibaada na ni lazima ukibisha kifo kinakuhusu Kwann ni lazima: kuna siku ya ibaada ambayo Mungu aliiweka kwetu sisi wanadamu nayo bili kuficha ni jumamos ndiyo siku inayomtukuza Mungu wa mbinguni na kumtambulisha kuwa ndiye muumbaji wa mbingu na nchi Kwa sababu ibilis naye anataka aabudiwe ameweka siku yake kwa wanadamu ambayo ni jumapili na mpaka sasa taratibu zinaendelea jumapili kuwekwa rasmi ni lazima uabudu katika siku hiyo hutaki kifo Lengo ni kuitoa sabato ya kweli inayomtukuza mungu na kubakiza inayomtukuza ibilisi Hizi agenda sasa ni kutafuta sababu mfano kuna agenda juu ya uchumi Kwamba eti watu wanakuwa na siku nyingi za kupumzika hawafanyi kazi hivyo uchumi unashuka iwekwe sasa siku moja ili watu wafanye kazi Ila ukweli sio hoja ni namna tu wapate kukubalika na habari yao ya kusimika jumapili kama siku ya ibaada na nyuma ya hili yupo ibilisi mwenyewe kwa kutumia mawakala wake hasa kanisa katoliki kwa uongozi wa papa.
Mwenyezi MUNGU akutie nguvu mtumishi wake, maana watumishi wengi hawalijui hili japo kuwa MUNGU mwenyewe amesema sana na wateule wake!... Huu sio muda Wa kuangalia dini wala dhehebu, sikiliza ujumbe na kuufanyia kazi muda umekwisha.
Kuhubiri unahubili lakini wewe nawe unaisujudia sanam ya mnyama bado upo kundi hilo tuuuh fanya uamuzi wewe kwaajili ya neema uliyo pewa na Bwana ukweli unao uchaguzi niwako usiwendeele kudanganya watu ingali unajua utakinywea kikombe chaazabu Bwana akubariki ufanyapo maamuzi 🙏🙏🙏
Kuna wakati nahisi Yesu alisharudi Ila sasa nikijiona nipo humu na mimi 😢 huwa naogopa sana. Tupambane sana sana maana kuumbe kwa upande mwingine utajiri wa wasiomjua Mungu ni sawa na kumwaga maji katika Gunia.... Hata na mataifa makubwa!
Neema ya mungu iwe juu yako mtumishi wa mungu tupo vijana tunao tamaani kuwelewa haya mungu akupandishe viwango nasi tupate kuelewa zaidi k.t.k jina la yesu
Mtumishi wa Mungu Mungu akubariki aweke ulizi juuyako maana maaduwi niwengi unavofichuwa Siri hizo Mungu akubariki na Mungu atufikishe salama huku tuendako!
Mpango wa ibilisi ni kutaka aabudiwe hivyo anaenda kinyume na Mungu kwa kila jambo Mungu alisema ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke Shetan yeye hata mme na mme wanaweza oana Mungu alisema ibaada ni siku ya saba Shetani yeye hata siku ya kwanza ya juma ni sawa tu So tuko vitani na vita ni kati ya wema na uovu ni kuchagua upande ni wapi usimame kwa Mungu au kwa shetani
Nakuunga mkono hakika..maana ni watu wengi wasioweza kufasili habari za mnyama... asante MTUMISHI WA MUNGU ALIYE HAI... ALIYE NA SIKIO NA ASIKIE AMBAYO ROHO AYAMBIA MAKANISA
Luka urukavyo Ufunuo 1:16-20 Yesu alikuwa na kinara na kinara kina vinara saba na juu ya kinara nyota saba, vinara ni makanisa na Nyota ni malaika kwa hiyo Bwana Yesu Kristo kwenye mkono ambayo ni mamlaka yake ana malaika saba ambao ndio Yesu aliwatuma ndio macho ya Mungu waonaji Manabii kwa kila wakati. Ufunuo 5:6 ndio waliotumwa Dunia huu ndio wakati wa mwisho kanisa la Laodikia kila mtu ni mjuaji ni ngumu Mungu kuwasaidia 3:17 ni vipofu uchi kanisa lina kelele nyingi. Lakini Mungu alisema Malaika wa saba (mjumbe) Ndio ATAFUNUA Ufunuo 10:7 nje ya Hapo unaswa ila ujui kama umenaswa mnyama waliwadanganya wakubwa kwa wadogo, Tajiri na maskini. itakuwa kama kuja kwa kwanza Yesu Kristo alivyo wakuta Mathayo 23:1_34Je hao hawakuwa wahubiri na viongozi wa dini je walimkubali Yohana Mbatizaji, je Walimkubali Bwana Yesu Kristo.
Kama sisi ni viumbe wa Mungu na tumeubwa na Mungu hatutaweza kuweka hofu juu ya maroboti maana tunajua kua Mungu alietuumba ndie anaetuongoza juu ya rizki zetu.