Mm binafsi ni muislam lakini Daniel mgogo namfatilia mwanzo mwisho. Uyu mzee ni moto wa kuotea mbali. Hua namfananisha na #Dida wa masham sham kwa kuipa jamii mabomu ya wazi wazi. Mungu awajaalie
Huyu mchungaji kiukweli haya mazungumzo yake nime yaelewa maneno mazuri ya kweli mashallah Allah amuongoze na amtie ktk dini ya uislam heshima kwako mchungaji.
@@danfordmilagiro1836 ni kweli maneno yako. Mm ni muislam lkn napenda sana kusikiliza mahubiri ya huyu pastor. Kuliko wengine kwa kweli. Allah amlinde na amzidishie elimu
Yani nyie waisilam huwa mnataka vitu vizuri viwe vyenu wakirisitu Wana mungu Alie hai na hawatangazi dini wanamtangaza mungu Alie hai Wala hawapiganii dini
Huduma ya kuponya ndoa na kuwaandaa vijana waheshimu ndoa na kujiandaa kuitika wito wa Mungu ni muhimu kwa sababu ndoa ndio taasisi kwanza aliyoianzisha Mungu. Ni takatifu kwa sababu aliyeanzisha ni Mtakatifu. Taasisi ya kwanza kabla ya anguko la mwanadamu. Ndio msingi wa jamii na mataifa. Kuanguka kwa familia ni anguko la jamii na taifa. Kutokana umuhimu huu na kusudi takatifu la Mungu, Shetani anapiga vita ndoa hataki iwepo. Na halali akiona ndoa yenye msingi wa upendo wa Mungu. Anaharibu amani na uaminifu ndani ya ndoa anazuia wazazi kuwapa watoto upendo, ulinzi na kuwajengea maadili ya kumcha Mungu. Tendo la ndoa si takatifu kama alivyotupa Mungu kwa ajili ya uzao na umoja wa mtu mume na mtu mke kuungana kuwa mmoja. Siku hizi hakuna seclusity na fidelity, kijana anafanya ngono kabla ya makubaliano ya ndoa, na wenye ndoa hutoka nje kutembea na wengine. Ukweli ni kwamba ngono haifanyiwi majaribio; ndio maana kuna ubikira; kwa sababu tendo hilo linaunganisha wawili, mwanamke na mwanamume katika wito na huduma ya ndoa ambapo mwanadamu anatakiwa kutii mpango wa Mungu. Kwa bahati mbaya wanadamu tumemwasi Mungu; sasa tendo la ndoa limegeuzwa kuwa biashara au kazi ya kipato. Wengine ni mradi kuajiri mabinti kufanya ngono kwa malipo. Ni unyanyasaji wa kiroho kisaikolojia na kimwili. Kwa wanaume wengine ni ngono ni starehe kwa hiyo hayuko tayari kwa matokeo ya mimba wala matunzo na malezi. Wasichana hawafundishwi kuthamini na kujivunia ubikira wao. Kwa sababu hii wako tayari kuingia agano la kumwaga damu na mtu ambaye hataishi naye. Ndoa sio mkataba bali ni agano. Na hakuna agano pasipo damu. Wanawake wengi ndoa zao hazina amani kwa sababu hazikufungwa kwa agano la damu, waliimwaga kwa haramia mpita njia. Kwa hiyo ni muhimu kuhakikisha kuwa vijana wanaoingia makubaliano ya ndoa inapasa kwanza kutubu kwa Mungu na kila mmoja kwa mwenziwe, maana waliuharibu ubikira na kusababisha kuimwaga damu ya binti(fulani) nje ya ndoa na kuruhusu kumwaga damu ya agano (na mvulana fulani) Suluhisho ni Lazima wote wafanyiwe deliverance na mtumishi mwenye Roho Mtakatifu ili kuondoa pepo la uzinzi na ugonjwa wa premarital sexual syndrome ambayo isipoondolewa kuna uwezekano wa kukosa uaminifu (seclusity na fidelity) yaani kuwa mwaminifu na kutosheka na mume wako mmoja na mke wako mmoja si kwenda nje. Wawili hao wakifanyiwa ukombozi hakutakuwa na tatizo la kutofurahia tendo la ndoa. Tendo la ndoa ni ruksa kati ya mwanamume aliyefikia muda wa kubeba jukumu la familia na kuwa na upendo ulio wa kimungu na Mwanamk e aliyefikia umri wa kujipambanua na kuwa mke/mwenza; mama wa kusimamia familia atakaye jenga maadili ya watoto watakaokuwa raia wema na kuwa utukufu kwa Mungu na fahari kwa jamii. Shetani anaondoa dhamani na utaķatifu wa ndoa. Ameleta kwa kasi roho ya usodoma yaani wanaume kuoana, kutoa mimba, kuzuia kuzaa na ndoa za mwanamke kwa mwanamke. Huu ni uasi; ni kwenda kinyume na Mungu. Tuiponye jamii tuwekeze kwa watoto na vijana wetu.
Dunia imefungwa katika mafumbo mengi,, Maneno ya Mzee ni mafumbo ,,,,na tabia ya watu ni kusifia mambo mazuri ila wamefichwa kujua yalio mema mbele za Mungu ....Behold Yeremia 4:22 Mungu atusaidie
Diamond hata asaidie ulimwengu mzima hana radhi ya baba yake ni lazima kwanza akaombe radhi na amsaidie mzee Abdul mzee Mkanye sio babake wala hafanani nae.