Wapendwa Mungu awabariki Kwa kufuatilia vipindi vya mchungaji kapola, Wengi tunalalamika kuhusu kingereza mwanzoni na Mimi nilikuwa nalalamika Ila Sasa nimegundua kuwa Ana waumini wa mataifa mbalimbali nilikutana na mzambia mmoja akaniambia Kwa lugha Yao akasema nanukuu, napenda kumsikiliza huyu mchungaji Kwa vile anavyochanganya na kingereza huwa naunganisha ujumbe najikuta naelewa anachofundisha. Kutoka pale nilipata Somo nikaacha kulalamika kuhusu swala la kuchanganya lugha
Swala hapa sio namna gani nimefurahi kusikia Mchungaji wangu anapigiwa simu na Rais, swala ni namna gani Mungu amelipokea hili la kupigiwa simu madhabahuni na ukasitisha maombi ukapokea simu, When we are in serious prayer, we are in call with our God who is above men and above all calls.
Mchungaji vipi tena ubadilishe lugha?hapo ndipo tunakwama waTanzania,ndiyo maana mama anasimamia kwenye kiswahili hajataka kuongea hiyo lugha lengo na washirika wasikie nini unaongea na mama, pia na mama anasemaje wasikie. Maana siyo washirika wote wanajua kiingereza.Binafsi sijapenda kiukweli.
Huyu pastor huwa anachanganya lunga ila kiingereza ni kingi kuliko Kiswahili, na waumini wake wengi ni vijana wa vyuo. Na kama muumini haelewi kiingereza ya nini kwenda kwake? Makanisa ya Kiswahili asilimia mia yapo kibao
maisha mbona magumu ajira akuna watu wanatekwa mnaombea kitu gani sadaka?? labda ombeni upungue ugumu wa maisha wachungaji acheni ukibaraka njaa kirakona sasa mnaombea nini uoga wenu nfio zambi zenu watumishi wa pesa
Adi Raha Yan mh siku Moja namm anipigie tu simu nahisi nitakujaga kuzimia cm ya mh rais dah nakupenda sana mama naomba siku Moja uniarike ikulu mama nikuone tunifulahi mama nakupenda sana mh rais wangu ila ndoivo elimu ndosina na Kaz kufika huko kazi
Ninachoona Mimi Kwa macho yangu ya mbali ni kwamba mama anatengeneza mazingira ya ushindi 2025 kupitia kula mtumishi mwenye watu wengi. Siyo jambo baya ni zuri sana sana rais kuthamini ibada za maombi na kuona umuhimu wa kuombewa na kuombea inch. Lakini watumishi mue makini sana, wana siasa wanatumia akili nyingi sana kujipenyeza madhabahuni Kwa ajili ya mambo yao binafsi.
Chochote ambacho mheshimiwa raisi atafanya kitaathiri jinsi wapiga kura wanavyomtazama. Yeye si wa kwanza. Waliomtangulia mara kadhaa waliongea na viongozi wa dini. Kuna viongozi wa dini wamejitokeza kumkashifu raisi na kukitukana chama cha CCM hadharani. Utayasikia askofu anasema CCM ni chama cha majambazi na matusi mengine . Anaongea huku amevaa T sheti ya chama cha upinzani. Sasa inatokea kanisa linaiombea nchi yetu, linamuombea raisi wetu kuna ubaya gani raisi kuwatia moyo kwa kuwapigia simu na kuwapongeza. Kati ya mahitaji makubwa kuliko yote ambayo raisi wetu anahitaji toka kwa waumini ni kuliombea taifa na kumuombea.
,Sio wote ni mapasta, wengine usalama so mnaposali hapo mnasali kikanjanja, Janja Janja ya kukusanya kura, yaani hii ni namna ya kutafuta kura kirahisi unaambiwa ukishaweza kuuteka ufahamu wa mtu basi kila kitu kwako kitakuwa mteremko, hapo anacheza na Akili za watu na walivyo wapumbavu wala hakuna anayeelewa kinachoendelea, tujifunze kusoma nyakati
Watanzania tuache ulimbumeni wa lugha za kigeni,Rais wa nchi anaongeo kiswahili,wewe unaongea lugha ya kigeni Ina maana Gani!!! Hivi ukienda kijijini kwenu wale bibi zako nao unaweza kuongea nao lugha za kigeni??? Tubadilike,kingereza ni lugha kama ki.............tu.