Akizungumza na maelfu ya Wananchi wanaohudhuria Kongamano kubwa la Operesheni Washa Taa linaloratibiwa na Boniface Mwamposa wa Kanisa la Inuka Uangaze, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda amewataka watanzania kuwakataa watu wanaotumia Neno la Mungu na mavazi rasmi ya Viongozi wa dini katika kuwarubuni Watanzania na kujinufaisha kupitia maandiko matakatifu.
"Ukimuona mtu yeyote mwenye jina au nafasi yoyote ya kidini lakini umaarufu wake hautokani na kazi ya mikono ya Kristo, hautokani na kazi za Mungu na za neno la Mungu, jua huyo ni Kiongozi wa dini feki. Nikupe mfano unielewe, Apostle Mwamposa hapa kamtaja Yesu Mwanzo mpaka mwisho, mmejaa hapa mnashuhudia kazi za neno la Mungu kupitia kinywa cha Mtumishi wake aliyepakwa mafuta kwaajili ya nyakati hizi, Heshima aliyonayo ni ya kufanya kazi ya Mungu ambayo sisi ni mashuhuda wa Matunda na maandiko yanasema mtawajua kwa matunda yao." Amesema. Makonda.
20 сен 2024