Jeshi la Polisi limeombwa na familia ya Bangala inayoishi Mburahati, Dar es Salaam kuwakamata wahusika wa kifo cha kijana wao Leonard mwenye miaka 31 aliyedaiwa kuuawa na askari wa Polisi Jamii maarufu (Sungusungu) usiku wa kuamkia Julai 10,2024 kwa madai ya wizi.
Marehemu anadaiwa kufuatwa nyumbani kwao na Sungusungu hao majira ya saa 9 usiku na kumsihi atoke nje kwaajili ya mazungumzo lakini hali ikawa tofauti kutokana na kile kinachodaiwa kufungwa kamba na kuanza kupigwa hadi umauti ulipomfika huku wahusika wakiwa bado hawajakamatwa.
@official_jennifersumi
29 авг 2024