Stephane Aziz Ki amefunga #hattrick Yanga ikiiadhibu Tanzania Prisons magoli 4-1 kwenye mchezo wa kuhitimisha msimu #NBCPremierLeague 2023-24 uliopigwa Azam Complex, Chamazi.
Waliotangulia kufunga ni Tanzania Prisons kwa goli la beno Ngassa dakika ya tano huku Aziz akifunga magoli yake dakika ya 11', 12', na 79' huku goli lingine likifungwa na Kennedy Musonda dakika ya 52.
Magoli haya yamemfanya Aziz kuwa mfungaji bora wa ligi #TopScorer akifikisha jumla ya magoli 21 mbele ya Feisal Salum aliyemaliza na magoli 19
Tazama highlights....
27 май 2024