Karibu katika Ukumbi huu wa Mawanda ya Lugha ya Kiswahili ambao unaangazia vipengele vyote vya lugha kwa mjibu wa mtaala wa elimu nchini Kenya vikiwemo uchambuzi wa vitabu vya fasihi andishi, fasihi simulizi, mashairi, matumizi ya lugha na insha. Hata hivyo, ni lengol letu kuwa wote wanaokienzi Kiswahili wanufaike katika ukumbi huu. Kutana na wanajopo wa ukumbi huu ambao ni walimu wenye tajiriba ndefu ya ufundishaji na utahini wa Kiswahili katika shule za upili nchini Kenya. Jopo hili linaongozwa na ndugu mwelekezi mwalimu John Nyandwaro kutoka shule ya upili ya mseto ya Nyarongi, Migori (0725625733), Mwalimu Dorin Chan-shule wa shule ya upili ya wasichana Kadika,Migori (0712962427), Mwalimu Silanus Migiro kutoka Shule ya upili ya Mseto ya Opolo ,Migori, (0701095183), mwalimu Don Oiriga wa shule ya upili ya wasichana ya Moi Suba, migori (0725362484), Mwalimu Mokua kutoka shule ya upili ya Rapogi (072133351) na wengineo.
Kazi kuntu wanajopo.Mzidi kuwa mwanga katika tasnia hii. Nawarai mfanye uchambuzi wa riwaya ya NGUU ZA JADI sura baada ya sura.Mtemi wasalimu Dada Chan,Kaka Don Oiriga Mnenawazi,Salanus Migiro.Nyinyi m wa maana sana.
kazi nzuri ila katika utangulizi mwasema '' karibu katika uchambuzi wa riwaya ya....'' hii ni hadithi fupi na wala sio riwaya. nadhani ni haraka ya uandishi
@@mawandayalughatv halafu nikuulize mwalimu, serikali inaeza nikubalia nirudie form 4 mwaka ujao ,,juu nilifanya form 4 2020 na ninataka kurudia kuna uwezekano
Baadhi ya hoja: Madhari haya yanaendeleza maudhui ya uharibifu wa mazingira-Makutwa anachimba migodi bika kujali usalama wa mazingira. 2. Yatumiwa kujenga sifa za wahusika-kwa makutwa ni katili, anashirikisha vijana katika uchimbaji migodi badala ya kuwa shuleni. Nk..