Mheshimiwa Rais Dokta Samia naomba utafakari muenendo wa wasaidizi wako. Sisi Vijana tunaenda kuleta Mabadiliko kuanzia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na ndiyo mwanzo wa anguko la CCM. Vijana maisha yao yamekuwa magumu sana na Nchi inanufaisha wachache. Vladimir Putin wa Russia na Xi Jin Ping wa China wamesema Changes is coming to Africa na Kenya wameanza kuonesha njia
Mbona Paul Makonda alivyokuwa Dar es Salaam hizi kejeli za Wakuu wa Wilaya hazikuwepo. Hata Mkuu wa Mkoa Chalamila inabidi awajibike haiwezekani Wasaidizi wako wanakurupuka kunyanyasa Wananchi
Chama cha Mapinduzi kinakosa Imani kwa Wananchi. Inabidi tuwe na Katiba mpya ili tuwe na mfumo wa Majimbo ili Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wawe wanapigiwa Kura na Wananchi. Sasa unakuwa Mkuu wa Wilaya Kijana lakini unapenda kuona Vijana wenzako waliokosa Ajira Serikalini wanajiajiri bado unataka kuwaharibia mifumo ya utafutaji. Hili halikubaliki
Wanyonge wakianzisha pakishanoga mnatutoa,tukigundua dhahabu serikali inampa muwekezaji tukigundua mashamba mara utasikia tokeni tunataka kuweka hifadhi,ukiwa karibu na bara bara ndio baraha unaambiwa bomoa eneo la Tanroad,muda mwingine serikali ata kama Wananchi tumekosea muweke ubinadamu.kwanza kwa Allah kunahukumu..
Huu ulimwengu wa sasa ni mtiani mkubwa ukiwa unapinga mambo machafu ambayo kuna watu baazi Wana manufaa nayo utapigwa kila sehemu hii Ndio Dunia ya leo unafki Ndio pesa kuwa mkweli unakuwa maskin
Huyu Mkuu wa Wilaya ni kijana lakini hana uzalendo mara avamie Guest za watu usiku wa manane, Chama cha Mapinduzi kibadilishe mfumo kama chama cha China Communists Party yaani kuwa Mwanachama tu unapewa Usaili angalau itapunguza kuwa na Viongozi wenye mihemuko kama huyu