Amejitahidi sana awe hazungumzib kwa kutumia maneno ya Kiingereza, na akitamka neno kwa Kiingereza basi amesahau maana yake kwa lugha ya Kiswahili. This is fantastic, tofauti na watu wetu wengi, Kiingereza kingi na hawakijui
Wewe ni mtangazaji nguli sana! Kongole kwa kazi ambazo unafanya! Mungu akupe heri na kukufanikishia yote! Big up sana Salim Kikeke Umeonyesha uzalendo kurudi nyumbani kurudisha na kuchangia katika taifa lako!! Pongezi sana kuonyesha muhimu na dhamani ya kazi yako. Kuwepo nyumbani tu inaonyesha na pia inawapa nguvu wale ambao wanadharau kazi kama yako!! nenda na msimamo huo wa kuonesha na kuelimisha jamii na wengine kuhusu dhamani ya kazi yako na pia mabadiliko ya mwajiri na mwajiliwa. Karibu sana nyumbani.
“Voluntary Redundancy” kwa muda aliotumikia BBC kuna malipo ambayo mwajiri anamlipa mwajiriwa au unalipwa pale tu mwajiri anapokubali ombi lako. Na malipo yanategemea na umri wako na muda uliotumikia, kwa Iyo Kikeke hajarudi mtupu kuna Maokoto yake mfukoni yanamsogeza sogeza katika muda huu alioamua kuja kupambana nyumbani, Well done Kikeke
Nakupongeza sana Mr Salimu Kikeke kwa uamuzi wa kurudi nyumbani. Wengine hudharau kwao kwamba Ulaya ni bora. Wewe ni mfano wa kuigwa. Karibu sana Tanzania tujenge wote nchi yetu.
Wajat sijaja ulaya nilimuomba Mungu sana nipate kazi uku ila tangu nifike ulaya namuomba Mungu sana nilud Tanzania sema mkataba unanibana Yan ndugu zangu wote kila siku nawambia jmni Tanzania ni kuzur mno maisha ya uku ni magumu cjawah kufurahia kuish uku
One of the best interview.. Yametemwa madini Sana, nmependa ubunifu, kuanzia kwenye intro ya uyo dada, ilo beat na utulivu wa show...Kikeke toka aondoke BBC sifatilii tena Dira ya Dunia.
Yani mwanadamu ukiwa Africa unapachoka ukienda ulaya unapachoka ukila sana ni shida, ukiwa na njaa ni shida ,,,raha pekee na amani na tulizo lipo ndani ya YESU KRISTO tu
Karibu nyumbani. Naipenda nchi yangu. Nami ni mmoja wa wake wanaopenda nyumbani. Hata hapa Tz maisha mazuri yanapatikana na furaha na mengine mengi Mungu aliyotupatia au kutupendelea sisi wakushi. Mungu fundi. Mungu ibariki Mungu ibariki Tanzania. Usiogope maisha yanaenda tuuuu
Wasanii na watu mashuhuri kuna cha kujifunza hapa; Salim licha ya kukaa Uingereza miaka 20 bado anatumia lugha moja kwenye mazungumzo. Sijasikia popote akichanganya Lugha ya Kiswahili na Kiingereza. Kuna kubwa la kujifunza hapa. Hongera Salim.
Vizuri sana Salim, kuna vitu viwili kwetu vinatupa utambulisho mbaya sana sana kwa watu wengine 1.Kujali 2.Kuthamini Washahili yapaswa tujizoeze kuja muda, kuja makubaliano, kujali fulsa. Pia kuthamini kitu cha mtu, kuthamini utu wa mtu, kuthamini chako na cha mwenzako. Mwisho kutambua!
Well said, lakini kumbuka kupuuzia mipango mingi ya kupata pesa wakati huna kazi ya kueleweka! Kwakufanya hivyo utafurahia sana maisha ya Nyumbani Tanzania.
Sio kweli jamaa unasema Tanzania ũkĩwa huna hela unakuwa mpweke? Nakataa sasa si watanzania wengi si wangekuwa wapweke sana? Kinacholeta upweke mkubwa tz ni watu kutaka kuishi maisha ya kupita uwezo au viwango vyao,mfano hapa dar watu wengi wanaishi kwa upweke sana maana wanapenda kushindana kwenye nyanja Za maisha ,kutaka maisha ya juu na kuishi Kuliko kipato chako ni sababu kuu ya upweke.lakini ukisema kukosa hela sio kweli maana asilimia 80 ya watanzania wanategemea Kilimo na Kilimo kuna MUda wa kusubiri ilĩ mazao yakomae sasa unadhani inakuwaje
Upo vizuri sana kaka salim, binafc nmeanza kukuckiliza Redion ukitangaza ktk idhaa ya BBC, ulinifanya nikawa siachi kutembea na karedio kadogooo, ilimlad tu nikuckilize ukitangaza mpira wa wingereza, pongezi sana kaka🎉
Sababu sio za msingi sana .ila kwa kuwa kaamuwa .kila pahala watu wanaish life style yao kila eneo dunian.maisha ya ulaya na marekan kama unapata kaz utakiw kuwa mvivu..maana muda wa kupumzika n mdogo sana ..na BILLS za kutosha .hakuna kukwepa kwepa kama huku .
Yani ningekua nimeshakusanya ela nyingi ningerudi Tanzania maisha ya ulaya no ya upweke sana, kikubwa ningebaki tu na Access ya kwenda na kurudi tu kwa ajiri ya kutibiwa tu na vacations
Kheri zaidi mtu kuenda nje kwa ajili kupata msingi wa kipato na mabalozi wanastahiki kuwa saidia wananchi wa tanzania wanapokwenda nje ya nchi kuwasimamia kupata ajira kwa wale ambao wanapata tabu ktk suala la ajira ili unapofika mda wa kurudi baada miaka wawe wameshapata misingi ya kimaisha kama mzee kikeke apo na wengneo
Ukimwambia mtu aliyeko afrika kwamba ulaya kuna upweke anaona unaongea nini wewe??mi napata pesa yangu nzuri sina muda kuwaza upweke😂😂😂😂😂😂usilolijua ni kama usiku wa giza
interview nzuri na location nzuri ila MILLARD izo wired mike ni very local,itashusha taasisi kwann msingeweka meza na avae wireless mike?,,lifanyieni kazi hilo sio mtangazaji mkubwa ashike maiki mkononi mwanzo mwisho,mmemkosea
hongera sana mtangazaji unayehoji maswali, hakika unauliza maswali kwa umakini na utulivu sanaaa. hakika una utulivu wa kiuandishi. fanya hivyo kwa wengine hadi kwa makamu wa raisi.
Kwanza Mr Salim Kikeke wewe ni mfano wa kuingwa na unaroho nzuri sana unaroho ya kusaidia wenzako na Allah Subhanallahu wa Taala anakuwezesha tunamshukuru kwa kutunuku hilo na tunamuomba aendelee kukujalia kila la kheri. Na wa Tanzania viongozi wa juu tambueni umuhimu wa huyu mtu muhimu kwetu aweze kupata nafasi ya kudumu ya juu hapa kwetu aweze kuwezesha watoto/wajukuu wetu kupata alicho nacho
Ila suala kutunza ahadi wageni wengi hulalamika juu ya Wtz kutokutunza ahadi pindi wanapo ahid kukutana na mtu mwingine, lingine ambalo bovu ni customer care ni mbovu mno
Safi Kikeke ila mandevu hayo hayapendezi kabisa yanachukiza sana. Hebu naomba uyakate kisha hiyo canter uiweke kichwani kwenye nywele. Ni ushauri wangu kakangu nakupenda sana hasa ulivyokuwa ukitangaza big up!
Millard Umetisha sana Huyu dada anayeongea Voice Over yuko vyema sana, nadhani maskio yangu ndio mara ya kwanza namsikia Mwanamke akireport katika Media yako. Kongole sana
😂😂, salm twambie ukwel, sema hivi nimefanya kaz kwa muda mrefu kila nikitaman kua mtu mkubwa mwenye pesa nashindwa nikaamua Nije Tanzania kutoka na kias cha pesa nilicho nacho nikirud tz ni pesa ya kutosha😂😂😂😂😂
it's very wonderful podcast, very inspiring however improve on your podcast gadgets such as mic, why holding a mic for over 30 minutes? it does'nt look more professional.
Upweke au maisha ya Upweke nimoja ya sabau zinazo sumbua sana watu wanao ishi mbali na nchi zao. Maisha bila kuwa karibu na familia au ndugu zako pamoja na marafiki wako nivigumu kufurahia kuishi nje ya nchi. Kuongea na ndugu au marafiki zako kupitia simu haitoshi, kuna muda unaitaji ata salamu ya kugusa mtu kwa mkono, kukaa na kuongea na marafiki zako ana kwa ana. Nimeishi nje/ China wakati wa corona Upweke kidogo unifanye kicha. Maisha Bora na ya furaha yako hapo hapo ulipo nyumbani kijijini kwenu kuliko kwenye nchi za watu. Mungu akutangulie S.Kikeke tunajivunia watu kama wewe. Wale tunao ishi nje ya nchi tukkumbuke kuwa nchi yetu inaitaji msaada wetu ili kuendelea na kutoa maisha ya kiwango cha juu kama maisha tunayo kimbilia kutafuta kwenye nchi za watu. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa.