Lilikuwa suala la muda kwa Mchungaji Peter Msigwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Ndivyo unavyoweza kueleza baada ya kada huyo wa zamani wa Chadema kutimkia katika chama hicho tawala.
Msigwa ametambulishwa kuwa mwanachama mpya wa CCM leo Jumapili, Juni 30, 2024, mbele ya wajumbe wa halmashauri kuu ya chama hicho (NEC), katika kikao kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Samia Suluhu Hassan.
Uamuzi wa mwanasiasa huyo umethibitisha tetesi zilizokuwa zikiibuliwa mara kwa mara na wadau zikimhusisha Msigwa na CCM, tangu enzi za utawala wa Hayati John Magufuli.
26 авг 2024