Huyu Mpina Anapaswa kuungwa mkono na watanzania wote. Lakini watanzania tusipoamka na kupinga mafisadi kama hawa ambao mpina amewafichua. Basi nchi yetu itazidi kuwa masikini kupindukia.
Siyo rahisi kutoka kwenye usingizi tulionao la sivyo tuwapate vitukuu wa mganga wa Nyerere watuelezee kile kifimbo cha Nyerere alichokuwa anatembea nacho, kinasemekana kuwa na nguvu za ajabu...na kifimbo hicho kilitumika kutupu..... hadi leo
Mpina kamungu siyo mtoto kufa Kwa mkilisto ni sawa na hama duniani kwenda mbinguni usiogope wezi wazima Hana nguvu jitowe ccm uwa ukweli hawataki watu wa kweli wanataka wapiga makofi usikubali
Hata kama mpina umesema kweli subiri utaratibu ukamulike. No a single tree can make a forest. Hao masikini unaotetea watakutosa, hawana maana kama hutumii utaratibu na sheria , si unakumbuka akina mrema alivyokua anabebwa, desi walipokusanyika nk. Mnyonge hana kinyongo mpina, mnyonge akipewa pesa anakutosa mheshimiwa mpina
Aiseee hali ni ngumu sana . Pesa nyingi sana znapigwa nchi hii ndiyo maana tunazidi kuteseka . Mungu wa mbinguni tukuinulia macho tunaomba usikilize kilio chetu . Wewe Mungu uonae yanayo yanayofanyika gizani tunaomba ubatilishe mipango yote ya hawa maibilisi .
Watanzania wanahitaji kumtetea. Maana wengi hawana uthubutu wakuweka wazi madudu yanayoendelea maana kiukweli ye yote anayethubutu hupotezwa ama kupata kama yanayoyompata Mpina.
Mpina haba kosa lolote ilq Viongozi wa Ccm hawataki kukosolewa hatufuati katiba inavyosemq ya Ccm Kiongozi qsiyekubali kukosolewa hastahili kuwa kiongozi soma katiba humo Bungeni unafiki umetawala sanaaaa wabunge ndiyo ni wengi sanaaaa wamuache Mpina na bado kila kitu kitakuwa hadharani
Hii ndiyo njia nzuri inayoshinikiza uwajibikaji serikalini. Madhali aliyoyaibua ni ya kweli, ni vizuri ameyaleta kwa wananchi ili waujue ufisadi uliomo serikalini! Isingelikuwa sahihi kwake kumsubiri spika auambie umma kwa vile inajulikana spika hatafanya hivyo, yupo pale kuilinda serikali hata ikifanya maovu! Na ushahidi wa hilo upo bayana!! Kumtaraji spika aliyewekwa na executive (ikulu) kusimama kidete na kuuambia umma wa waTZ ukweli ni kupoteza wakati kwa vile yeye anawajali waliompa u spika!
Mhe: Mpina mimi nimetokea kuwa shabiki wako pale ulipojitokeza kuchukuwa nafasi tuliyoikosa kutoka kwa wabunge wa upinzani, ila naanza kuwa na mashaka juu ya msemo niliokuwa nausikia ukisemwa "SIASA NI MCHEZO MCHAFU" Nisiwe mnafiki nahisi ni mpango mahususi wa chama chako!?? Ila kama ni msimamo wako nakushauri utoke huko uungane na wenye hoja hizo..!
watanzania ufahamu wetu wengi ni mdogo sana Mpina alikuwa na hoja ila alitakiwa awasilishe kwa taratibu zilizo wekwa hata kama una hoja fata taratibu tusiwe wajinga
Pale ambapo ni dhahir taratibu zimewekwa kimizengwe ili kuficha maovu ya serikali, ni bora kutozifuata taratibu za namna hiyo! Nahisi wewe usiyeng'amua hadi sasa kwamba hakuwezi kutokea uwajibikaji TZ kwa kufuata TARATIBU zilizopo, basi wewe ndiye mjinga na unatuchelewesha! Bila kuziruka taratibu hizi zilizojaa kulindana, huwezi kubadili chochote popote!
Kwanza bunge lenyewe ni haramu uwepo wake umetokana na kuvuruga uchaguzi 2020 kinyume cha katiba.je wale wale wabunge 19 wa chadema uwepo wao umefuata sheria?spika hovyo sana.