Safari ya maisha ya Jasmin kutoka Tanzania na kuhitaji kuingia Ulaya kutafuta maisha
Alipata mchongo wa safari ili akifika Ulaya aweze kujilipua lakini mambo yalienda ndivyo sivyo na kuishia kua Deported akiwa ametua tu Ufaransa hata nje ya airport hajatoka.
Na alipoingia Ulaya mara ya pili basi aliishia kuingia Jela nchini Ugiriki ambako alikaa huko kwa muda wa miezi sita.
Mtanzania mwenzie alimuingiza mkenge na kumsababishia matatizo makubwa kwa kumuibia passport yake.
Lakini hakukata tamaa aliamua kutafuta mbinu za kumtoa Ugiriki ili afike Ujerumani na hivyo alianza michakato ya safari za ukumbizi ambayo haikua rahisi na ilikua na changamoto nyingi na kuishia kukaa jela tena katika nchi ya Albania na Macedonia
Kwasasa anaishi Ujerumani na anafanya kazi huko.
Thank you Jasmin for allowing this to be online
www.oda.international
13 мар 2024