Arusha sijui baridi au vipi, mbona kama haya matukio yanaongezeka kila kukicha, mi ninachojua mortuary wanapewa majina kamili ili wamuandae mtu wao kwa kidhibitisho, mbona kama mnatuchosha, hii inawahusu wote mortuary attendant na familia
Kuna sababu ya kuona mwili unapooshwa wawepo wenye marehemu. Kwa nini? Waosheji wanafanya kilankitu pasipo ndg wa karibu ndio maana mambo haya yanstokea
Uzembe mkubwa hospital, juzi tu mjombaa kaonekana mzima wakati mmezika mtu, viongozi wa hospital mnazembea sana, kila mwili kila mgonjwa anaingia na jina lake inakuaje mnachanganya majina ya maiti au majina ya mgonjwa uzembe wa hali ya juu hatua kali zichukuliwe
Ni Yale Yale ya Yule kaka yaani haya mambo huku yapo sana lakini utashindwaje kumjua ndugu yako? Bora sasa wametambua mapema au tuanzishe utaratibu Wa kuvalisha wagonjwa bangili zenye majina huko hosptali