RC Makonda ni mbunifu sana. Alipokuwa mkuu wa mkoa wa Dar alibuni namna ya kuwasaidia waalimu wa shule kusafiri bure na alifanikiwa. Anafaa kuwa kiongozi japo wapo wanaompiga vita kwamba anaingilia madaraka ya wengine
Kuna mambo watanzania tunajiuliza kwani mh makonda ni peke yake tu mkuu wa mkoa nchi mzima au mbona mikoani hawawezi kuiga hiki kizuri anachofanya huyu mkuu kwa faida ya wananchi km mikoani kungekuwa Moto km Huu jmn Nani angelalamikia serikali na wakuu wengine waige Basi mazuri ya makonda kwa faida ya nchi na wananchi wake.naomba kuwasilisha.
Jaribuni tu kumpa nafasi ya kugombania nafasi ya kugombania urais, nitampa kura zangu zote ambazo niliacha miaka kama ishirini na tano iliyopita kupiga.Yangu ni dua na maombi tu, si mnaona anavyofanya hapa Arusha.nchi ni uongozi bora tu, kila kitu tunacho.
Tatizo Wakuu wamikoa wengine kabla yakua Wakuu wamikoa walikua Wakuu wafamilia zao kwaiyo wanaongozwa nahofu yakushambuliwa wao nafamilia zao kama ukipata nafasi yakumuuliza Makonda anayo yapitia kama unamoyo wafamilia Yako na Ndugu zako inaweza ukajiuzulu siku hiyohiyo kwakua Makonda ukiacha Kuteuliwa Na Raisi Kateuliwa Na MUNGU ndio maana unaona anafanya Hayo anayofanya ila Vita anayo pitia Nikubwa kuliko Umri wake ila Kwakua Mungu ndio kamteua ataendelea kufanya hayo anayo yafanya nakama Mkuu Wamkoa yeyote ataiga basi hatochukua raundi maana Vita nikubwa sana Tena sana Mungu aendelee kumlinda nakumtunza maana ni Hazina ya Taifa Mungu Mbariki Makonda Mungu Ibariki Tanzania
Makonda anafanya kazi vizuri,anajua maisha halisi ya mtanzania wa kawaida,anajua mateso ya wananchi,sio mbinafsi na anaupendo wa kweli na hofu ya MUNGU ,tumuombee sana kwa M MUNGU aendelee kumlinda na ipo siku ataikomboa Tanzania, MUNGU ambariki sana mh Paul Cristian Makonda 🙏🙏🙏
Ashe Oleng.Mkuu wa mkoa nakuheshimu sana.umeshafanya mengi mazuri hapa kwetu Arusha. ombi langu ni hili tuongezee muda kwenye hili kambi, watu wengi bado hatujawaona madaktari.
Unafanya kazi nzuri sana kiongozi , Ukitoka kwenye Afya Mh , uje na hukukwenye usafi wa mazingira Arusha , magari ya kukusanya uchafu mjini zinatembea zikidondosha uchafu mji mzima mpaka ikifika dampo gari halina uchafu ni vibobo tu vya chupa za maji kwa ajili ya kwenda kuuza wao wafanyakazi . Mamlaka hazisimamii ipasavyo
Orchidopexy inafanyika na masurgeon au Urologist Surgeons au hata madaktari wazoefu kwa hivi zinaweza kufanyika mikoani huko huko wala si tatizo geni la kuhitaji Muhimbili tu. Na elimu itolewe kwamba wazazi wachunguze watoto zao na wawahi kabla ya miaka 5 ambapo inakua rahisi kufanya Orchidopexy
Hivi si wachukue madaktari wapasuaji wachache wafundishwe wakafanyie mikoani kwao? Halafu wala si operesheni ngumu ya kumshinda general Surgeon au hata daktari mzoefu. Kuhusu kula nyama sidhani Arusha Nyama inauzwa bei rahisi hadi wengi kumudu kuinunua na kula mara kwa mara.
Kiuhalisia ni ubunifu mzuri sana wa RC. Lakini, tujiulize kwanini watu wanajaa kwenye kambitiba hivi? Ni kwasababu wengi wao huenda walishindwa kulipia gharama za matibabu hayo kwenye utaratibu wa kawaida wa tiba kwani wengi hawana hizo bima, au vifurushi vya bima hazikavi baadhi ya garama za matibabu na vipimo vyao. Inamaana watakuwa wanasubiria hizo kambi ili kupata matibabu ya Bure au ya bei nafuu ambayo serikali inagarimikia kuleta vifaa na madaktari? Na je, hawa madaktari huku kwenye vituo vyao vya kazi inakuwaje? Nashauri utaratibu wa bima uwekwe Sawa, ili kuondoa uhitaji wa makambi ya tiba na watu waendelee kutibiwa hospitali kama kawaida?
Serikali ingeweza kuweka huduma za afya bure kwasababu mfano Leo Mgonjwa anatibiwa anapata Dawa je akimaliza Dawa Muendelezo wao unakua sio Mzuri kutokana na ugumu Wa upatkanaji Wa huduma na gharama za Dawa na huduma kwa ujumla
Hizo kambi zinaweza kusaidia watafiti kukusanya Data ambazo zinaweza kutumika kwenye uandaaji wa Bajeti ya Wizara husika. Lakini pia inaonesha changamoto ziko mahali gani.