DAR ES SALAAM: Rais wa Guinea-Bissau Umbaro Sissoco amesema yapo mengi ya kujifunza nchini Tanzania haswa katika suala la maendeleo ya Miundombinu.
Sissoco ameyasema hayo wakati akitembelea Reli ya Kisasa SGR ambayo imemfikisha Pugu kutokea Stesheni jijini DSM.
Akiwa ndani ya Treni hiyo ambayo imempeleka hadi kituo cha Pugu na kurejea amemweleza mwenyeji wake umuhimu wa kutembelea nchi ya Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ziara hiyo Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile amewataka watanzania kujivunia mazuri yanayotekelezwa na viongozi wao, huku Mkurugenzi Mkuu wa TRC Masanja Kadogosa akieleza namna Reli hiyo inaumuhimu kwa mataifa hayo mawili katika kukuza uchumi.
21 июн 2024