Mheshimiwa hizo nchi unazosema wanalipa kodi angalia na usimamizi wa kodi zao. Huenda wananchi wao wanaona kodi zao zikisimamiwa vizuri, zikifanya makusudio, haziendi mifukoni mwa mafisadi. Tuige kupigana na mafisadi ili walipa kodi walipe kwa furaha!
Mpendwa Rais wetu, hebu waambie maafisa wetu wa kodi waende Uganda wakajifunze kama URA wanapambana na wafanyabiashara. Tuna tatizo kubwa la rushwa ndio chanzo ya yote
Pamoja na mgomo uliotokea mama tra bado ndio chanzo cha maradhi ya watanzani sukari presha hawapend kuona maendeleo ya mlipa kodi mishahara yao wanaokula kutusumbua sisi itatoka wap?
mama Samia sikutegemea, i thought you would stand and let others follow suit and pray for our Jirani Kenya. they are our strategic business partners, when peace is restored in their quarters happy are we au?
Siyo kwamba watu hawataki kulipa kodi, wanataka lakn tatizo ni pale tunaposikia mabilioni yameibiwa, ambazo ndizo hizohizo kodi. Dhibiti mianya wa wanaoibia serikali ili walipa kodi wawe na imani na kodi zao kwamba haziendi mifukoni mwa watu.
Shida sio kulipa kodi mama. Tatizo ni hawa wakulungwa wako unao waweka kwenye hayo makusanyo ya kodi wanapiga tu sasa unapatia wap nguvu ya kulipa kodi
😁😁MAMA ANGU MPENDWA CHUNGUZA HAWA VIONGOZI WAKO AMBAO KILA WAKISIMAMA WANASEMA TUNAPENDA KUMSHUKURU MAMA SAMIA hao ndo chanzo cha yote sijui wenyewe wanafanyaga kazi gani
Mama wewe ni kiongozi bola kuwaikutokea nchini kwetu semanini kunamijitu inapenda kupelekwa kipundapunda nawewe ni mchamungu mwenyezi mungu atakulipa kwamema unayoyafanya inshallah wewe ni raisi bola apa nchini kwetu watakukumbuka utakapomaliza mudawako endelea kututumikia watanzania tunakupenda Sana mama kazi iendelee
Mama Samia, kodi unapandishia wa/nchi wako bila huruma. shida hiii hela mbona hatuoni kinachofanyika? viongozi wako wanakula sana kutokana na ww kusema kuleni kwa urefu wa kamba yako. kodi tulipe sie kula mzitafune nyie, deni la taifa kkuongezeka, miradi unajitaidi lakini hiko ktk viwango stahiki..haki hakuna nchini na bibilia inasema Haki huinua nchi..mbona husikilizi vilio vya nchi yako Mama?
Mama cheka na nyani wananchi tunavuna mabuwa wanakusifia mama kaupiga mwingi na maneno matamu matamu ya kukupamba alafu wanakuibia wanakungongaa kisogo