Тёмный

Salama Na SAMATTA SE6 EP49 | HEADMASTER PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460 

YahStoneTown
Подписаться 395 тыс.
Просмотров 133 тыс.
50% 1

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kila kijana wa ki Tanzania ambae anaupenda na kuuthamini mpira wa miguu na ambaye angependa ndo iwe kazi ya maisha yake basi Mbwana Ally Samatta ndiye role model wake, hakuna doubt kwamba watakua na mapenzi na Cristiano Ronaldo au Leo Messi au Kylian Mbappe au Marcus Rashford ila yule ambaye amewaaminisha kwamba INAWEZEKANA ukacheza POPOTE hapa duniani na hasa kwenye ligi yetu pendwa ya Uingereza ni Samatta. Rafiki tu kutoka Mbagala rangi tatu ambaye kashacheza saaana ndondo na makombe ya mbuzi wakati anakua na mwisho wa siku akaenda kucheza kwa wazungu na bado anaendelea kutafuta rizki yake huko, hata kama sio ligi ile ambayo hata yeye mwenyewe angependa awepo ila BADO ni MWAMBA wetu. Samatta huyu huyu ndo ambaye alijitwika mpira kichwani na kuitika nyavuni mbele ya beki ambae anaaminika kuwa BORA kwa misimu hii miwili mitatu ndani ya Virgil van Dijk. Hata wakati naandika hii bado mwili unanisisimka kwa wazo tu kwamba nililishuhudia lile, pata picha kwa mtoto ambaye ana ndoto hizo. Lile goli lilimfanyia NINI kwenye ndoto zake. KRC Genk walipoteza mchezo ule wa ugenini wa kombe la mabingwa wa Ulaya kwa magoli 2-1 ila kwenye mitaa yote ya mikoa ya Tanzania ile mechi ilikua ya USHINDI.
Mbwana ametokea kwenye familia ya kawaida sana sana, wazazi wake wote kama kumbukumbu yangu itakua 100 basi walikua polisi, najua kwa hakika Baba yake alikua Polisi kwa asilimia 100. Kwa marehemu Bi Mkubwa wake ndo sina hakika sana ila kwa hakika jibu limo kwenye haya maongezi yetu. Anakumbuka jinsi ambavyo Mzee wake alikua anasisitiza kwenye suala la elimu na heshima, kama mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, Mbwana aliupenda sana mpira, zile za kujiiba na kwenda kucheza mechi za mbali alishafanya sana na matunda ndo haya ya leo. Nadhani ilifika kipindi Mzee mwenyewe aliona basi sawa, twende huko utakako. Familia yao yote ni wapenzi wa mpira na Kaka yake Mouhamed bado anacheza hapa hapa Tanzania. Sasa akiwa kama kioo kikubwa sana kwenye jamii hii Samatta anazungumzia presha ambayo hupewa hasa pale anapoitwa kwenye timu ya Taifa, jinsi maneno mengi ya kashfa yanaporushwa kwake kutoka kwa wananchi na anakumbuka pia wakati bado anacheza T.P Mazembe kuna kipindi kocha aliacha kumuita yeye na Rafiki yake Thomas Ulimwenguna ilisemekana kama pengine hakuna na interest na team au hakua anatoa 100. Pengine kipindi hicho aliumia zaidi maana hiyo haikua jambo zuri kwake.
Mbwana anazungumza na mimi kuhusu urafiki wake na Ulimwengu na maisha ambayo walikua wanaishi pamoja wakati wako DRC, anakumbuka jinsi walivyokua wanapanga kufanikiwa pamoja na mipango yao endelevu kwenye career yao. Ulimwengu nae ana siku yake kwenye kiti chetu In Shaa Allah maana nae ana mengi ya kutuelezea. Majeraha ya mara kwa mara bila ya shaka yalisababisha kwa kiasi kikubwa ndoto zake za kucheza Ulaya kutochukua hatua ya juu kama ambavyo angependa, ila mimi naamini hayo yote maisha tu, kila kitu kilikua tayari kimesha andikwa.
Samatta ni Baba ambaye watoto wake wanasoma hapa hapa nyumbani, nilimuuliza kama watoto wake wanajua yeye ni nani na akanipa story ndogo ya yeye kung’amua kama wanafahamu fika Baba yao ni nani.
Mwenzangu humu kuna mengi sana ambayo yatakufaa na kwa nafasi ya kipekee ningependa kumshukuru Captain wa Taifa kwa kuchukua time kwenye ratiba yake ambayo ilikua imebana kweli kweli ili tu aje kutubarikia meza yetu kwa uwepo wake.
Yangu matumaini uta enjoy sana.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪RU-vid Link bit.ly/RU-vidSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Развлечения

Опубликовано:

 

8 янв 2023

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 134   
@mbwanamtessa8607
@mbwanamtessa8607 Год назад
Kama bado unamkubali huyu jamaa gonga like twenzetu
@Jibambeshow254k
@Jibambeshow254k 5 месяцев назад
Santa very humble and peaceful guy naona ananyayo kama za Ali hana mbwembwe and that's why he's unique ❤hii sampuli ndio kio cha jamii
@rashidchimwenda
@rashidchimwenda Год назад
Big up kwa Salama kuweza kutuletea Samatta. Anaongea mambo mengi mazuri ya mfano kwa vijana wetu kwa soka letu. Ila suala la maadili sikubaliani naye aliposema ni yeye mwenyewe. Bila shaka maadili yake mazuri yamejengwa ktk familia yao (baba na mama) na hususan kwakuwa ni familia ya kipolisi, timu alizopitia hapa bongo na tamaduni zetu za kitanzania. Sisi watanzania tupo vizuri kimaadili kuliko baadhi ya watu wa mataifa mengi. Kila la heri kwake na Salama.
@chiconinde8135
@chiconinde8135 Год назад
Baada ile ya Jakaya....Hii tena umefanya kubwa Salama🙌⚽️💪
@arafajabir3194
@arafajabir3194 Год назад
Mungu amempa uwezo ila hapendi show off anaishi kama Ali kiba good bless you
@nellymatalanga5033
@nellymatalanga5033 Год назад
You are ths two people wamebarikiwa but wako humble na down to earth
@mzirairebeca9996
@mzirairebeca9996 Год назад
Nature ya kazi yake pia
@mzirairebeca9996
@mzirairebeca9996 Год назад
Ukiwa msanii makelele hayakwepeki
@silvanusremmy9575
@silvanusremmy9575 Год назад
Sasa Alikiba ametokea wapi. Acha makasiliko 😀
@samniza1763
@samniza1763 Год назад
The first ever sensible young Tanzanian born and raised in Tanzania. Proud of who you have become.
@JJ-sx7ne
@JJ-sx7ne Год назад
Labda wewe kingereza hakipo kabisa! 98% kaongea kiswahili..
@sawaabyahya584
@sawaabyahya584 Год назад
Huyu mwanamme mbona best baba! Ni kioo cha jamii..... Vijana wajifunze kupitia tabia yake.... Ahsante Salama kumtafuta...
@majomamajoma8776
@majomamajoma8776 Год назад
Nina mwanangu anakupenda na anacheza mpila hatari Huwa anajiita samata, sapoti wanetu vijijin kaka nao watimize ndoto zao Allah akufanyie wepesi uzidi kung'ara
@com5766
@com5766 Год назад
The best interview Hey kenyans give likes for it
@deospackle2158
@deospackle2158 Год назад
Samatta anasound humble sana🔥🔥🔥
@hanssenbensonmturi2435
@hanssenbensonmturi2435 Год назад
Ulivofanya interview na Idris, nilitamani ufanye na Samatta as well. Nilivyoona hii leo, ilinikosha sana kwani Samatta ni nguli na role model to a lot of us young footballers. I am currently playing my football in The Thailand 3rd division and I dream one day not only to replicate the legend’s work but also I dream of being part of this show. Thank you Salama and Samatta for this wonderful interview
@Chemba67
@Chemba67 Год назад
Keep it up Hanssen Benson.......your name sound Danish.......
@allahisone6386
@allahisone6386 Год назад
@Hanssen God bless you ❤️🙏❤️
@shwaibukhatibu2838
@shwaibukhatibu2838 Год назад
SAMATA NA KING KIBA ALLAH BLESS YOU OTHER CELEBRITIES THEY HAVE TO COPE FROM YOU
@stevewanga957
@stevewanga957 Год назад
Hes very humble like Ali Kiba...much love from🇶🇦🇶🇦
@mnasicafe1319
@mnasicafe1319 Год назад
Yeah
@GodfreyPaul
@GodfreyPaul Год назад
Much appreciation for your popa🔥🔥🔥
@albogastmselejr4583
@albogastmselejr4583 Год назад
Aiseh! Jamaa Mbona Haongei Kingereza Kama Mimi Wakati Mimi Nimekaa Week Tu Nime Sahau Kiswahili 😁😁
@jackbujimu3220
@jackbujimu3220 Год назад
🤣🤣🤣🤣 mie nimesoma tu English medium primary Ila mpka Sasa ninachanganya ngeli Kama nimeish mambele
@mussachabonga9595
@mussachabonga9595 Год назад
Fantastic interview big up sister Salama 2023
@RehemaChap3
@RehemaChap3 5 месяцев назад
Samanta MUNGU akubariki sana una busara sana
@tatutumbi4640
@tatutumbi4640 Год назад
Salama Hongera Sana. Nafatilia Sana Vipindi Vyako. Navipenda. 👍
@erickchitumbi1308
@erickchitumbi1308 Год назад
Mbwana unayo hekima na busara sana.safi sana.
@rosemofuga8101
@rosemofuga8101 Год назад
Waoooooo fantastic mr Samatta
@homan_nkwama
@homan_nkwama Год назад
kama baadhi ya majibu yanatakiwa Sana ili kutimiza mahojiano ni sawa ila kama sivyo, naomba salama punguza kujenga MASWALI yanayo mlazimu mtu ajibu katika mtazamo fulani.....awe huru tusitarajie atajibu nini I LOVE YOU SALAMA
@ayubuakko9495
@ayubuakko9495 Год назад
Salama jabir Ur on 🔥🔥
@mofungoya9729
@mofungoya9729 Год назад
Best player ever ♥️🇹🇿
@luciasteven3314
@luciasteven3314 5 месяцев назад
Nimechelewa sn kumjua samatta❤
@januarysungura8119
@januarysungura8119 Год назад
Your the best not just of luck but you deserve it keep up samatta
@jojigeorige1056
@jojigeorige1056 Год назад
He's well programmed aisee
@mountaincoffee7
@mountaincoffee7 Год назад
Noma sana
@SaidiHassan-pq3zf
@SaidiHassan-pq3zf 4 месяца назад
Bless captain Diego
@andrewjulius2306
@andrewjulius2306 Год назад
Sam ✊🔨 keep it up bro unjua
@nomamatata754
@nomamatata754 Год назад
I keep saying salama you got best questions for your guests.....you keep asking my questions every time i get time to see your sessions.....be blessed girl
@marwajuma7493
@marwajuma7493 Год назад
Nilisubili Sanaa asante sanaa
@peterkichochi7510
@peterkichochi7510 Год назад
This Guy is very humble and smart, he knows how to communicate
@ahmedjaffari9375
@ahmedjaffari9375 Год назад
Exactly… he is truly a professional footballer, may Almighty Allah bless him abundantly 🙏🏿
@robinhomesuza8906
@robinhomesuza8906 Год назад
Naskia sauti ya ommy dimpoz zinafanana
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Год назад
Huna Baya bro
@user-xu2vg2ge2q
@user-xu2vg2ge2q Год назад
Uyu yomuli Dar Es Salaam Tz 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
@mweusiasili8345
@mweusiasili8345 Год назад
Capten Diego
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Год назад
Legend Bro
@moganfred6473
@moganfred6473 Год назад
Nakkubali sana
@furahambwembwe6935
@furahambwembwe6935 Год назад
Humble man...
@Revo_silayo
@Revo_silayo Год назад
Hyo ni nature ya intruvant peoples Huwa wanakuwa na rafiki wachche lkn wanapendwa na wengi na Huwa wanajifanyia maamuzi wenyewe na pia wapo focused na hutoboaa sanaaa.
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Год назад
Salama tunaomba ufanye interview na nadir haruob canavaro
@maishakisunzu391
@maishakisunzu391 Год назад
Kama umegundua lafudhi ya samatta ishabadilika automatically kuwa ya kiingereza gonga like hapa😝
@navigatorelias9794
@navigatorelias9794 5 месяцев назад
Wewe acha zako babu, Asa si lazima hiyo hata wwe ukitoka kwenu huko dongo kusimamia ukija mjini lazima kiswahili chako kibadilike, so sielewi unataka kumaanisha nn
@mrlabay9871
@mrlabay9871 Год назад
🔥🔥🔥🔥
@thefeyotz
@thefeyotz Год назад
Aliifunga Liverpool 😁😁
@hassanikipusa8328
@hassanikipusa8328 Год назад
Champion Boy 🇹🇿
@flavianchuwa4370
@flavianchuwa4370 Год назад
Waaaaoooh Asante kwa hii Salama
@dseven7094
@dseven7094 Год назад
mbagala boy
@safiyatheonlything7848
@safiyatheonlything7848 Год назад
leo salama na samata
@daggerslick
@daggerslick Год назад
Woyoooo mbwana samatta😜😜😜
@dullayomwinyi3359
@dullayomwinyi3359 5 месяцев назад
Mwamba huyu ni hatari sana
@edwardfaraji1133
@edwardfaraji1133 Год назад
Sama goal Sama Sama goal....
@mr.graphics3213
@mr.graphics3213 Год назад
Tz oneeee🔥🔥🔥🔥
@abuujuhayfa4321
@abuujuhayfa4321 Год назад
SAMATTA 🔥🔥🔥 gonga like kwa mwamba
@dreamfootballclip1096
@dreamfootballclip1096 Год назад
Home boi
@xnobmedia1
@xnobmedia1 Год назад
Dah Salama kwa kumleta salama umenitouch saaaana yan. Hebu pokea 10k la soda hapooo.
@kabirigisaidi8253
@kabirigisaidi8253 Год назад
Sama goal Sama goal. You de best bro
@ibraimoissiaca6058
@ibraimoissiaca6058 Год назад
Popa
@jamaalsaleem2926
@jamaalsaleem2926 Год назад
WA kwanza leoooooo
@hansigajijime4108
@hansigajijime4108 Год назад
Mwamba kabsa
@bish_daddiyao
@bish_daddiyao Год назад
Mimi mkenya Ila Huyu Jamaa namkubali🙌🏾⚽♥️⚽
@ramadhanmaisa788
@ramadhanmaisa788 Год назад
Hakun ulazim wa kusema ww n mkenya
@googleus4903
@googleus4903 Год назад
MWAKINYO ANGEPATA NIDHAMU NA HESHIMA KAMA YA NDUGU NYETU SAMATTA ANGEFIKA ZAIDI YA ALIPO LEO.
@tztanzania2262
@tztanzania2262 Год назад
Mbona na mwakinyo yupo fresh tu!
@barbarasara4033
@barbarasara4033 Год назад
@@tztanzania2262 dharau nyingi
@mickidadybakari9974
@mickidadybakari9974 Год назад
Mwakinyo mtu poa saaana kama utam chukulia poa ila kama ukiwa mduanzi utam hulia mbona ila ni mshikaji saaana tena zaid ya saaana
@aishaomarry6996
@aishaomarry6996 Год назад
Huyu ni mimi kabisa hua naamua mwenyewe mambo yangu.
@tztanzania2262
@tztanzania2262 Год назад
Usifanye hivyo mara zote jtahd baadhi ya mambo kuomba ushaur
@dmikepresenter
@dmikepresenter Год назад
Samatta Goal 🇹🇿🇹🇿🇹🇿
@MariamHamad-lr3xc
@MariamHamad-lr3xc 5 месяцев назад
Kipendacho moyo dawa
@donnietommie8444
@donnietommie8444 Год назад
#SalamaNaDrLeaky
@brunofernandez6608
@brunofernandez6608 Год назад
Samagoal Mbagala Boy
@FireHouse123
@FireHouse123 Год назад
Samatta mkali sana namkubali
@pheninhojr5875
@pheninhojr5875 Год назад
Samagoal #hainakufel
@kanyika14kanyika16
@kanyika14kanyika16 Год назад
SAMATTA anatabia kama zangu😁😁
@mwasagamwambuli3513
@mwasagamwambuli3513 Год назад
Mbwana you are what your father and mother groomed you to be what you are. Be appreciative of your parents
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Год назад
True
@FranklinMtei
@FranklinMtei Год назад
Was looking for this. Kajikuza mwenyewe? Heshima kwa wazazi
@anumario7footballlife936
@anumario7footballlife936 Год назад
Kaka yangu
@mdalamgir-gu9hu
@mdalamgir-gu9hu Год назад
Yan pia salama leo ujui umulize nn..
@nahyialetomia9284
@nahyialetomia9284 Год назад
Nafurahia wewe kujenga msikiti
@MariamHamad-lr3xc
@MariamHamad-lr3xc 5 месяцев назад
Wanasema pesa ni sabuni ya roho
@kulwamwakagali24
@kulwamwakagali24 Год назад
Champs Boy
@gasorekassim5499
@gasorekassim5499 Год назад
Kizaz san
@rehemambilinyi9452
@rehemambilinyi9452 Год назад
Tuletee na pastor Tony kapola,
@saumusalimuhassan2499
@saumusalimuhassan2499 Год назад
Laana ya wazazi ndio hiyo mitihani.
@cvanoedward3093
@cvanoedward3093 Год назад
Salama mbona watukatisha?
@samludo5435
@samludo5435 Год назад
Mlete mandonga salama
@henrymassawe699
@henrymassawe699 Год назад
😁🤣🤣🤣🤣😁😁😁😁 hatavuruga interview aiseee!!!🤣🤣
@abdallahmanula1627
@abdallahmanula1627 Год назад
Apo salama umenichanganya kabla amjaaanza nyuma muanze mbele mimi cjakuelewa kabisa
@walafredchikawe4113
@walafredchikawe4113 Год назад
😂😂😂😂
@albertbayona8441
@albertbayona8441 Год назад
Kwan jaman ilo neno shock mbona watu ulitumia vibaya
@Oldskulgemini9991
@Oldskulgemini9991 Год назад
SEMA hata wazungu hutumia Hilo neno mara nyingi Sana so Wala sio ajabu SEMA labda kwakuwa umeona wabongo pekee😅
@ahz6907
@ahz6907 Год назад
Linatakiwa litumikaje?
@kamanziian1073
@kamanziian1073 Год назад
Wewe ndo hulielewi
@kostasagelidis5326
@kostasagelidis5326 4 месяца назад
ωχχ ο σαματαςς χαχα
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Год назад
Bro umetupa funzo kubwa cc vijana, wewe nd mchezaji usie kuwa na wajivuno na nadir haruob Kwa maono yangu
@msuyatztv5201
@msuyatztv5201 Год назад
ru-vid.com/video/%D0%B2%D0%B8%D0%B4%D0%B5%D0%BE-bOC1NRBzhQA.html Ujumbe wa wafanyakazi Kwa Mama samia
@adamsengo1869
@adamsengo1869 Год назад
Wape points zao wazazi maana wao ndio source ya tabia yako
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Год назад
Masikito kua cjasikia hili kutoka kwake
@adamsengo1869
@adamsengo1869 Год назад
@@mashamassingisa8738 eti ni yeye tu amejikuta yupo ivo yani kama vile alijikuza mwenyewe, naona kama vile kwa mbali ana katabia cha kujimwambafai flani hivi
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Год назад
Masikitiko makubwa kk
@izzi198
@izzi198 Год назад
angevuta bangi na kuwa teja mngewapa point wazaz wake? Acheni kushinikiza ujinga
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Год назад
@izzi haya kk uko vyema sana
@Bam268
@Bam268 Год назад
Apo mnatuchanganya Birmingham ipi sasa ya gwajima au?
@eddiearts3713
@eddiearts3713 Год назад
birmingham ni mjini ndani ndio kuna club ya aston villa
@barbarasara4033
@barbarasara4033 Год назад
Nakojoa. ..... Kwa kucheka
@mdalamgir-gu9hu
@mdalamgir-gu9hu Год назад
Tatzo utembei nawala ulizi pia mitandao uoni
@denisruvugo1764
@denisruvugo1764 Год назад
Hahahahahahahahahahahahahahaha
@ibrahimshilinde6129
@ibrahimshilinde6129 Год назад
Kwani wewe Salam,Nani huaga anakushauri kuwakandia vijana wenye talent za mziki?
@tutumarzouk9803
@tutumarzouk9803 Год назад
mbona sama goal anajifanya kama hajui kiswahil vzr, yan kama ameish eurupe since he was childhood
@mdalamgir-gu9hu
@mdalamgir-gu9hu Год назад
Kizungu gan kazumgumza apo izo actualy nyingi..
@bryanlimbi326
@bryanlimbi326 Год назад
Sasa he was childhood ndo nini ..!? , Jifunze grammar mbwa wewe
@timmahbee
@timmahbee Год назад
@@bryanlimbi326 ilikua na ulazima wa kumtukana????
@noelsanga6853
@noelsanga6853 Год назад
@@timmahbee wivuuu tu unawasumbua
@anoldjefsta177
@anoldjefsta177 Год назад
@@bryanlimbi326 na aanze kubweka saivi
@jilalajr_official
@jilalajr_official Год назад
@samagoal77 #diego
@baritone_online_tv2565
@baritone_online_tv2565 Год назад
Noma sana
Далее
ЗАМУРОВАННЫЙ ФОКУСНИК
00:44
Просмотров 47 тыс.
Заячий Стон - Рот пятничный
0:55