Nchi zilizoendelea ambako treni za umeme zinapita hakuna hao ngedere. Wanyama wakikatiza, mfumo wa umeme umewekwa kwa namna ambayo utajikata Ili kutoleta madhara. Hivyo siyo tatizo la TRC hilo.
@@robertphilip385Wana kesi ya kuhujumu ya kuingia kutembea kwenye reli bila kibali (trespassing) hukumu yake kifungo miaka miwili jela kwa mujibu wa kanuni za sheria na kosa la kuhujumu uchumi (economic sabotage) kifungo miaka watapona kweli?
Shida moja tanzania uchawi mwingi ..na hurka ya mchawi apendi maendeleo...hakunaga kitu kizuri tanzania cha serikali kinacho dumu sijui kwanin....Mungu komboa tanzania
Ndiyo maana tunadumaa miakiliwa kuamini kila tukio baya.ni matokeo ya uchawi! Huwezi kujipa nafasi ya kitafiti chanzo cha tatizo unatumia shortcut ya uchawi kuwa kisababishi. Ni lini tutanipa uweo wa kutafakari mambo kimantiki? Hapa nilipo umeme umekarika mara mbili ndani ya dakika kumi, nao nu uchawi?
Kwa sisi Mafundi Tunakubali...changamoto kama hizi ni kawaida katika kazi...na tufahamu ndo kwanza kwa Treni kama hii kutumika Tanzania...Yatakaa sawa Tutakuwa wazoefu kadri siku zinavyokwenda...pole Wasafiri kwa changamoto hii.
Acha ujinga wewe, we need expert sisi tunataka mainjinia hapo hatutaki watu mlio ajiliwa kimichongo ili mje mjifunzie hapo KAZI uzoefu kachukue chuo ulkija hapo fanya kazi
@@JonasMathias-s6m, treni kama hizo ziko uchina , India , Uturuki nk nk nk je wanapata matatizo kama hayo?????! Au ndiyo kwetu tuuuuuiii !!!!!!!!’ KUNA VITU HAVIHITAJU UFUNDI KUVIJUA
Si kama kigamboni pantoni za Serikali mbovu za baharesa nzima ten oersent ssnhata Railway watapewa ten persent yabaki mabasi. Mwendokasi ataoewa muwekezaji akitoa ten persent yatabaki dala dala na mwendokasi. Barabara za mwendokasi Imegengwa bure reli zimejwngwa bure tren Itakuwa gest ya mjusi kafiri kenge.
Tanzania 🇹🇿 hakuna kukubali washamba wachache wasimamishe maendeleo. Kweli aliyetuloga waafrika keshakufa. Ni kuvunja laana uchawi, nguvu za giza husuda na kadhalika kwa damu ya yesu kristo. Waislamu ndugu pia ombeni sana kwa kumpitia Mtume Mohamed salalah wasalamu.
Matajir washaanza kulalamika mabas yao yanaenda matupu hayana abiria wakutosha kwaio wameshaanza vitimbi na hujuma watu warud kwenye mabas hakuna bundi wala ngere hapo nimpango kazi wa matajir flani hv 😅😅
Yaani! Na hata usafi tunaouona ni wa muda tu. Daladala zilianza hivi 1977, kulikuwa hakuna kusimama, mwendo kasi ilikuwa ya kwanza ya kistaarabu Afrika. Leo hii, daladala watu wanarundikwa, mwendo kasi watu kama samaki wabichi, kuambukizana magojwa, wanawake wajawazito wanabanwa. Watu wanagombania nani awe wa kwanza kupata kiti. Wazee na wagonjwa ni watu wa shida. Waziri wa usafirishaji bado hajiuzuru! Waziri wa akina mama na watoto bado upo? Zebra haziheshimiki tena, boda ndiyo usiseme kugonga watoto. Hivi sisi ni watu au fotokopi? Mbona Waganda na Kenya wamebadilika? Kwa nini kusiwe na vituo vya mafuta punguzo ili watu wawe kwenye level seats? Treni hii kwa ustarabu duni tulio nao tutegemee wajinga kuchafua soon!
Sio issue ya nchi bhana....Kama unadhani unaweza ku avoid all problems unajidanganya........ Labda uwe kaburini.... Unaweza kuwa serious na ukakumbwa dhahama vilevile.....
Hawakusema itaendelea hadi ifike kituoni, itaenda kama kilomita kadhaa tuu kisha umeme ukikawia itasimama. Jamani tuwe tunafatilia mambo vizuri. Lakini hata hivyo, hivi ni vitu vilivyotengenezwa na mwanadam, haviwezi kukosa itilafu. Ni jambo la kawaida tuu hilo tuwe waungwana kutosha.
Mtaomba radhi sanaaaa na bado mm ili niwapongeze baada ya mwaka C A G awakague aseme hakuna hasara ndo nitawapongeza sasa hv ngoja tuwaangalie tu niwaulize ile tren ya abiria isiyo ya umeme walipanda kina mond na pole pole iko wapiiiiii
Kwa hyo Mna mpango au mkakati gan wa utatuzi wa kudumu wa hili tatizo??? Au mtakua mnasubiri hao ngedere na Bundi wakisababisha short au wakinasa mkawatoe na kuwasha tena?????
Jaman ngedere usiku kweli hii hapana Trc acheni kufanya hujuma tunafaham wenye mabasi hawataicha train yetu bila ufumbufu lazima watashirikiana na wakati kuihujum train yetu.
Hapa inaonekana kuna upiga wa fedha za mafuta huwa wanaandikia mafuta hewa ya emergence kila siku endapo umeme utakata kama taarifa yao ya awali kuwa endapo umeme utakata mafuta yatatumika iliujue wamepiga kama kungekuwa na mafuta inakuwaje ikae saa mbili bila kwenda kama ni tatizo la umeme hawa huwa wanaandikia mafuta kila siku ila mungu kaamua kuwa umbua mapema kwa namna hiyo
Ili mradi mashirika ya serikali yatakuwa yanashindana na mashirika binafi, na mashirika hayo binafsi yanamilikiwa na viongozi wa serilali, basi kila wakati patakuwa na migogoro wa kimaslahi (conflicts of interests) mashirika ya kiserikali yataathirika tu.
Changamoto kama hizi ndo zitatukomaza kama nchi. Kwa mazingira yetu ya nchi na maeneo ambayo reli inapita ni vitu vya kutegemewa kuona wanyama au ndege wakigusa miungombinu ya umeme na kusababisha hitilifu kama iliyotokea. Lakini wahusika ni vizuri kufikiria jinsi ya kupunguza uwezekano wa wanyama hao kuingia au kufka kwenye miundombinu hiyo. Binafsi sioni sababu ya watu kupanic.
Mh isije ikawa kama Mv Kilindoni waliiuwa wakabaki na mitumbwi yao. Mzowea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi Hivi wabongo tutaacha lini uchawi ili watu wakate tamaa warudi kwenye mabasi yao, wanaanza kamdome kamdome. 😂😂😂😂advertising hiyooo.
Tutakuwa sawa tujue ichi yetu ndogo tusifananishe na ichi zilizojipanga na wameendelea miaka 50.b4 cc wengine kuja duniani izime iwake cc tunayo mama piga kazi sema kumtoa jerry silaa umetupiga na ki2 kizito
Umeongea kizembe sana kama vyote umenunua kutoka nj'e basi kopy na mfumo wa ulinzi na uendeshaji kopy kila unachoona kitakusaidia ili uwe salama na si kujiona we bado sana huku unaharibu
Elewa ndugu hilo ni tatizo tofauti, nyaya ndizo zilizochezewa na hao wanyama kwa hiyo hata kama ingekuwaje treni isingeweza kwenda kwa sababu zinapita chini ya hizo nyaya. Nyaya zikiwa sawa hata kama umeme utakatika kwa muda flani treni inaweza kwenda lakini zinapopita ndipo palipoharibiwa sasa itawezaje kupita?!
Haipiti chini ya nyaya, inapita kwenye trein nyaya zipo juu, pia walisema inahifadhi umeme wa ziada, maana yake hitilafu kama hizo zikitokea ilitakiwa iendelee kuchapa mwendo kwa saa nzima, wewe unasema ingepita wapi kwani umeambiwa reli imebomoka? @@rayisadesigns2646
kwa tulio fanya kazi sgr kilosa na kidete tunajua wingi wa ngedere , ni wengi hatari alafu ngedere wana utani hadi wanakera😅, sasa c changamoto itatokea kila siku
Sio kwelli.....kabisa. haiwezikani UKA unda kituo Cha kupooza umeme. Lakini usi zingatie madhara ya ngedere na bundi. Hizi ni changamoto tu za awali tunazo pitia tukizoea MFUMO. Huu kama raia nge sema kuungana mkono na uwekezaji huu APA mkubwa, tupo pamoja na shirika hili. Na tunge nufaishwa zaidi na winginwa report kutoka watu binafsi namna VIPI, usafiri huu ume weza raisisha au kuezesha maisha.
ila mbona kama walisema hata umeme ukizima,treni zina auto system ambayo itajibadirisha na kutumia mfumo mwengine hapo hapo ili safari iendelee.... ila sawa ili tuone panapovuja ni lazima inyeshe kwanza.
Kwa tabia hii ya ngedere na bundi kuchezea nyaya za umene wa reli ya SGR, nawashauri TRC watenge fungu kwenye budget yao ya kutoa semina elekezi kwa ngedere na bundi kuhusu umuhimu wa kutunza na kuthamini miundo mbinu ya SGR na hatari ya kuchezea nyaya za umeme. Vinginevyo watashitakiwa kwa kosa la trespassing na economic sabotage! Poleni abiria kwa adha, kadhia na usumbufu mliokabiliana nao!
Tulihakikishiwa ifuatavyo😢 Tanesco ikiwa na tatizo yafuatayo yatanyika: 1. Treni Ina backup power ya kwenda Dak 20 2. Kuna generator zitawaka na kutoa umeme 3. Injini Zina diseli ya kuiendesha. Sasa Kwa massa mawili hakuna lililofanyika. Kadogosa sema ukweli
Ngedere na bundi kweli ina maana haobundi ndio wamekuja leo ? Umeme haukuepo kabla ya bundi au ni baada ya bundi kuwepo.... HIVI MNAONA WATANZANIA NI MAFALA
Mnaposema Ni ngedere,Nyani au bundi mnamaanisha Nini?,Kwa maana hiyo Bundi ngedere au Nyani ndiyo wataamua treni iende au isiende!?, njooni na sababu yenye mashiko!!