Тёмный

Zuchu : "Nilipeleka Nyimbo Kama Tano, Diamond Alizikataa Zote" | SALAMA NA ZUCHU 

YahStoneTown
Подписаться 397 тыс.
Просмотров 134 тыс.
50% 1

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kuna usemi mmoja unaenda kama hivi, kulea mimba si kazi ila kazi ni kulea mtoto, tafsiri yangu naamini mhenga hapo alikua anatuambia kazi pengine inaanza baada ya kupata kazi, tunaelewa jinsi gani ambavyo kupata kazi huwa ni kazi. Tena kazi yoyote, haijalishi kama ni ya upishi au ulinzi au ufundi au hata u daktari, mi nawajua madaktari kadhaa ambao nao pia wanapata shida kupata hizo kazi. Na baada ya kupata shida zote hizo wakati wa kutafuta kazi basi kazi halisi huanza pale unapoipata sasa hiyo kazi yenyewe.
Kazi ya Zuchu ilianza kabla hajaipata hiyo kazi yenyewe na ilikua kazi haswa kuipata na Mama yake Bi Khadija Kopa ndo alikua kinara kwenye hiyo connection ambayo Binti yake alikua anaitaka ili aweze kuwa msanii wa Diamond, na hayo ndo yalikua maneno yake hasa, toka alivyorudi kutoka Nigeria kwenye mashindano ya kusaka vipaji na alikua hajielewi elewi kwa kiasi flani ni kitu gani alikua anataka kufanya na kama basi kutakua na la kufanya inabidi liwe kutoka WCB na sio sehemu nyengine yoyote na agulia nini kilitokea? WCB aliipata na kilichokua kinatakiwa baada ya hapo ni UVUMILIVU wa HALI YA JUU.
Kwenye vitabu vyangu vyote Bi Zuhura Othman Soud ndo muandishi wangu BORA wa KIKE kuwahi kutokea katika kizazi chetu hiki cha Bongo Flava, na naweza sema hivyo wakati wowote iwe usiku au mchana, kipaji hicho ndicho kilichonifanya mimi nistaajabu sana na kutaka kuongea nae na kumuuliza yote yale ambayo nilikua nataka kumuuliza, ingawa humo humo nilikua nishajijibu kutoka kwenye historia ya familia atokayo ingawa hiyo haikutakiwa ndo iwe lazima, lazima mtoto wa Khadija Kopa na Othman Soud awe muandishi mzuri maana wazazi wake wamejaa vipaji tena na Baba yake ndo muandishi mkubwa wa nyimbo nyingi za Mama yake zilizowahi kuvuma.
Kwa umri wake wakati mwengine hujiuliza kajuaje haya maneno yote, anajua maana yake hii? Kasikia wapi hili neno au pengine je huwa anamfikiria Mama yake (ambaye ndo kipenzi chake na ndo amemlea) wakati anaandika hii? Anaona aibu? Je huwa wanaongelea hayo mashairi wanapokua wawili tu? Mazungumzo huendaje?
Sasa turudi kwenye kazi hiyo ya kuanza kuifanya baada ya kuipata sasa WCB, ukiachana na msoto mrefu alopitia, WCB wenyewe walikua waangalifu sana kwenye mipango ambayo ilikua ikiandaliwa kwaajili yake, yeye ndo msanii wa KWANZA wa KIKE kuwahi kutokea kwenye label kwahiyo ukichana na kipaji pia uwekezaji wa hali ya juu ulitakiwa ufanyike and boy they did that. Toka single yake ya kwanza mpaka wakati naandika hii Zuchu hakuwahi kuwa na kazi chafu, album yake ya kwanza alotoka nayo ya I am Zuchu ilikua na nyimbo 7 ambazo zote zilienda kufanya vizuri, na mpaka leo kila wimbo ambao anaachia ni wa moto, tukisema namba moja nadhani namba zake pia zinasema hivyo za kila sehemu, hakuna chumvi yoyote ndani yake.
Vipi sasa anaweza ku maintain hii schedule yake ilojaa mambo kuanzia asubuhi mpaka usiku? Kutoka Jumatatu mpaka Jumapili? Je ana muda kwaajili yake? Ana mpenzi? Mipango yake je? Endelevu? Vipi hizi title ambazo tunampa anazichukuliaje? Kuna pressure yoyote? Na kuhusu familia je? Kuna pressure yoyote kwenye baadhi ya mambo na maamuzi? Na kwenye label nako? Watu na furaha na kazi yake?
Kwa kuanzia msimu wetu wa TANO nadhani introduction ya Ms Zuchu inatufaa sana na yangu matumaini uta enjoy pia.
Asante kwa support ya toka siku ya kwanza ulipoanza kutupa macho na masikio yako.
You’re the best, nakukumbusha tu kwamba mengi yajayo yatakufurahisha In Shaa Allah maana kazi ndo kwaanza imeanza.
Love,
Salama

Опубликовано:

 

5 окт 2024

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 183   
@elizabethmapunda
@elizabethmapunda Год назад
Napenda zuchu anavyoongea very charming😍
@nurutatu4031
@nurutatu4031 Год назад
One of the best interviews ever. Keep it up Salama and Zuchu👏🏽
@rosemahenge9071
@rosemahenge9071 Год назад
Hakuna kitu kizuri kama kuangalia interview ya mtu mchangamfu kama Zuchu 🥰🥰🥰
@kantai737
@kantai737 Год назад
For real her interviews are always a vibe Na she is really intelligent everytime ukiskia interview zake u can’t help but love her more.
@BigZhumbe
@BigZhumbe Год назад
Mimi interview hata iwe masaa kumi naimaliza.... Yeye na Simba they are great kwenye interviews
@MrTop-wj7no
@MrTop-wj7no Год назад
@@BigZhumbe umepatia kabisa
@isharsalim454
@isharsalim454 Год назад
🥰🥰
@mamananga2849
@mamananga2849 Год назад
@@BigZhumbe sanaaa
@handwatchmaro4124
@handwatchmaro4124 Год назад
Leo nmejikuta nampenda Zuhura😍 zaidi ya Zuchu
@zamzamsharif9776
@zamzamsharif9776 Год назад
ILike her she’s down to earth. Loove from Ireland 🇮🇪 ❤
@chancystv3138
@chancystv3138 Год назад
Watu wa Zuchu gongeni like hapa 🙌
@BigZhumbe
@BigZhumbe Год назад
Zuu you are great 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 simba jike umebebwa ukabebeka hadi wasafi waliokubeba wanaijoi na mashabiki tuna have fun.
@hamismkude553
@hamismkude553 Год назад
Nawakubali sana zuchu na salama kila mtu ana play party yake vzr yaan salama anajua kuuliza maswali na zuchu anajua kujibu maswali
@sarahlondo7597
@sarahlondo7597 Год назад
Aaaaw i love the way she is real❤️‍🔥🥰
@hopedj275
@hopedj275 Год назад
one of the best interview i have ever seen in my life
@elizabethotieno7270
@elizabethotieno7270 Год назад
Best interview ever,,,this girl is beautiful and wise
@hadiadaoman1981
@hadiadaoman1981 Год назад
Exactly even me I love her much more ♥️❤💖🥰
@maijamtoso5673
@maijamtoso5673 Год назад
Interview Nzuri mno.. inafurahisha na kufunzaa
@djibrilheradi8291
@djibrilheradi8291 Год назад
Happy for you zuchu,may Allah protect you
@SultanDean
@SultanDean Год назад
Salama be asking all the right questions
@fortune3502
@fortune3502 Год назад
Interview nzuri sanaaa! Daa nimekapenda bureee katoto ka watu jaman
@keyla3641
@keyla3641 Год назад
Zuchu akili nyingi usibadilike u are a good girl
@kantai737
@kantai737 Год назад
You just can’t stop loving her❤
@eveodera6676
@eveodera6676 Год назад
Salama this is one of the best interviews. I love the way your calm and Zuchu is just awesome.
@dayannahkopellah8396
@dayannahkopellah8396 Год назад
She is clever😇
@rehemaothman2475
@rehemaothman2475 Год назад
Majibu ya ukomavu nakukubali zuchu🥰🥰🥰🥰😍
@violetandisi
@violetandisi 10 месяцев назад
i just love salama for some strange reason she is so real i mean she asks the correct questions in a polite manner and zuchu love the energy girl and the wisdom
@mariammbaruk8034
@mariammbaruk8034 Год назад
Niliisubir xanaa hii zuchu love u😘😘
@goodlucksway1456
@goodlucksway1456 Год назад
👏👏👏yuko positive sana zuchu kama zuchu
@jacintabati6238
@jacintabati6238 Год назад
ZUCHU my love🥰😘😍❤❤❤
@africanbeauty6556
@africanbeauty6556 Год назад
Proud of you Zuchu!! Keep it up don’t change 🥰
@diva_20162
@diva_20162 5 месяцев назад
Her voice God waoooh so wonderful 😊😊
@mohamedrajab358
@mohamedrajab358 Год назад
Huyu binti yupo vizuri mno kwenye kichwa chake
@hadijasalim7769
@hadijasalim7769 10 месяцев назад
Zuchu hadi umeniliza mamy nakupenda❤❤❤❤
@monicajohn2515
@monicajohn2515 Год назад
Yani salama ana bonge la interview saaaana big up salama
@deborahcharles4916
@deborahcharles4916 6 месяцев назад
I love you zuchu haulingi dada
@stellah3844
@stellah3844 Год назад
Nakupenda Zuchu💓💓💓
@nyanziratatou5404
@nyanziratatou5404 6 месяцев назад
Ici kibindi nakipenda kwasababu hakina ushabiki kwata kwenye masali maswali yanaoulizwa yanajitosheleza . Kwakweli napenda da Salama.❤
@lulumalima1739
@lulumalima1739 Год назад
Nice much love and prayers from fellow Tanzanian women both you ladies
@allymakangana6450
@allymakangana6450 Год назад
salama ni muwazi sana sio mnafiki
@claricejoshua820
@claricejoshua820 Год назад
She is very humble nimempenda
@TheMullins830
@TheMullins830 Год назад
This girl just has some good energy in her. She sounds so sincere when she speaks.
@loiceamugune6711
@loiceamugune6711 Год назад
Salama you are one of the best interviewer
@jessicahjohnstone7229
@jessicahjohnstone7229 Год назад
Best interview
@MrTop-wj7no
@MrTop-wj7no Год назад
Interview nzuri Sana Kwa kweli,
@salimdibundile4872
@salimdibundile4872 Год назад
Salama you are the best... Tunakuomba utuletee kipenzi chetu mbosso khan
@zhaujiakashindi6617
@zhaujiakashindi6617 Год назад
🥰😘Love you Salama❤️
@DsonHadso3-kb1ue
@DsonHadso3-kb1ue Месяц назад
Zuchu is the best ever for me actually I like it's English very much
@princessiyalicious4185
@princessiyalicious4185 Год назад
Yeeee wakwanza mm leo
@estherjackson6038
@estherjackson6038 Год назад
Jamani mi naona maneno hapo juu nyuma ya Zuchu,KumaNoko Kula, au sioni vizuri.
@SiziniPrimary-yt1mp
@SiziniPrimary-yt1mp Месяц назад
No my dear hio ni kuonja ndiko kula 😊
@lynawamahoro3465
@lynawamahoro3465 Год назад
I like … wise one 👏
@jabirsuleiman26
@jabirsuleiman26 Год назад
I like it 🎉
@kimah9461
@kimah9461 Год назад
Ikitajwa diamond platnumz zuchu ni mgin🙈🤣👏🤣🤣🤣Is all❤️ beautiful MashaAllah Keep going sis
@kantai737
@kantai737 Год назад
😂😂😂😂😂
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 Год назад
Salama with her trick questions eti kwa vile SIMBA aliruka na wanawake wengine ukiwa na mimba 🤣🤣🤣🤣
@vincentmushi1247
@vincentmushi1247 Год назад
Ukisikia watu wanalalamika kuwa eti Mtu Anaongea kiingeeza wakati wa interview... Ujue hao watu hawajaenda shule...hahahaaaa, Kama unaelewa hauna muda wa kulalamika.. Ndio kiswahili ni lugha yetu na kiingeeza ni lugha pia... Nendeni tuition mkavunje yai jamani
@jasmineedamu6089
@jasmineedamu6089 Год назад
Achana na sisi😏
@fatmazullu4933
@fatmazullu4933 Год назад
@@jasmineedamu6089 🤣🤣🤣🤣
@minzamariamcasmir189
@minzamariamcasmir189 Год назад
Kweli kabisaa….watu wanabidi waelewe she’s an aspiring international artist if not one already so she needs to be accessible to everyone
@keyla3641
@keyla3641 Год назад
Hahaha nimeinjoi sana asante salama
@Jay47tz
@Jay47tz Год назад
Interview nzuri sana
@matanohassan9667
@matanohassan9667 Год назад
Nakupenda zuchu
@vanessaphamarcy2134
@vanessaphamarcy2134 Год назад
Nimekupenda buleee unahekima kaza but
@johariasanimatu2732
@johariasanimatu2732 Год назад
Zuchu my blood 🥰🥰🥰
@sebastianmwakulya8146
@sebastianmwakulya8146 3 месяца назад
Nimeangalia tena na tena hongereni sana kwa interview
@NafisaHeradi-o1z
@NafisaHeradi-o1z 9 дней назад
Zuchu nakupenda 🎉
@gknifeboy9435
@gknifeboy9435 Год назад
Gud interview
@kellymutabesha1876
@kellymutabesha1876 Год назад
Katoto kana akili mingi njomana simba kadata
@JohariLushemeza
@JohariLushemeza Месяц назад
Your are very zuchu...❤
@suroorAlafifi-ve8pk
@suroorAlafifi-ve8pk Год назад
Will see beautiful woman and I amazing thang 🥰 the best way to be careful about it and nice 🙂
@shilahshilah6136
@shilahshilah6136 Год назад
Mie ni mkenya lakini nampenda zuchu sana,,,,ningepewa nafasi nimuone tu ningeshukuru
@rosemarysiame8443
@rosemarysiame8443 Год назад
Jamn jaman this was funny jamn if you have crush with someone ooooh my god it's very jamn kafeeling kale duu
@yvespungu3611
@yvespungu3611 Год назад
Nice interview
@ismailebani5262
@ismailebani5262 Год назад
Safi Zuchu
@vincentmushi1247
@vincentmushi1247 Год назад
Interview nzuri... Na hongereni wote... Zuchu Aka chuchu... Hapo kwenye ku date na simba... Hahahaaaa. Ni Swali gumu sana... Biggest mistake... Zuchu ni mtulivu lkn simba wetu bado ni kicheche.
@dilipdab3714
@dilipdab3714 Год назад
English.ipo.poa.lakini.salama.yupo.fresh
@franciskajessy4468
@franciskajessy4468 28 дней назад
Interview nzuri sana🙏
@abdulraufmohammedsalum6806
@abdulraufmohammedsalum6806 Год назад
Salama🙌
@AfricaYangu
@AfricaYangu Год назад
All went well until u ask her about Diamond that's when she started behaving like a little girl
@successconcious703
@successconcious703 Год назад
😂😂😂😂💔💔
@veronyanganda179
@veronyanganda179 Год назад
Mafanikio ya zuchu nyuma yake kna watu sahihi wa kwanza mama yake, na mpenzi wake daimondi.
@fatmasaid3536
@fatmasaid3536 Год назад
Kwajili ya kiki, she's been trained ili atakapo ulizwa kama anam date simba ajifanye shy ili ionekane kuna something kwa mtazamo wangu hamna lolote ila kiki tu.
@khadijahali4837
@khadijahali4837 Год назад
Weee hamna lolote kwl hy?
@esthermusanga8118
@esthermusanga8118 Год назад
Also me I wish you all the best
@remybuyenzi1856
@remybuyenzi1856 Год назад
❤❤❤❤
@aslayhassan2283
@aslayhassan2283 Год назад
I like it
@maulidmalik5364
@maulidmalik5364 Год назад
Jaman sjaona msosi leo
@nyotakaminkya714
@nyotakaminkya714 Год назад
J'aime tes paroles ina saidia mipango iliko kichwani
@CecyliaEdward
@CecyliaEdward 2 месяца назад
I love zuchu and diamond
@mohamedjuma1878
@mohamedjuma1878 Год назад
Ma Ami Leo mmekutana
@oxtinho159
@oxtinho159 Год назад
Wa kwanza
@PrincessHellen-pg1oy
@PrincessHellen-pg1oy Месяц назад
Nice interview 👌 😊 ila baba zuchu kamkosea sana lakini ndo ubinadamu
@RadjabuIngabire
@RadjabuIngabire 13 дней назад
Salama unaweza
@NabakiZanzibar
@NabakiZanzibar Год назад
Kuipata hii ni bahati sana,
@arnoldmangi2407
@arnoldmangi2407 Год назад
Iko poa sana
@marianusrutagwelera3013
@marianusrutagwelera3013 6 месяцев назад
Nice sr zuchu😮
@lareineminah1353
@lareineminah1353 Год назад
Mme kawiza kuyitowa La simba lisha kuwa waziiii🤣🤣🤣
@esthermbike3300
@esthermbike3300 Год назад
Wema sasa
@donraykiko4243
@donraykiko4243 Год назад
Kwaiyo kiswahili mpemba kinampiga chenga au ndo tunakomoana tu
@stephanocyprian2892
@stephanocyprian2892 Год назад
Pamojasana zuch
@husseynomar9523
@husseynomar9523 Год назад
Salama tafadhali tuleteeni SHEIKH MUHIDDIN MAALIM SIASA NA SABRA MACHANO WATU ZANZIBAR
@mwanatz5980
@mwanatz5980 Год назад
😍😍😍
@mariamandambike5013
@mariamandambike5013 3 месяца назад
Zuchu🔥🔥
@nelialomnyaki
@nelialomnyaki 5 месяцев назад
Nimependa kingereza cha zuchu
@kidungweshaaban9317
@kidungweshaaban9317 Год назад
hujampa hat juice why!?our zuchu!!
@KSJ6569
@KSJ6569 Год назад
Iyi nimarudiyo sio mpya
@anitakamene4656
@anitakamene4656 Год назад
Nice
@mvponlinetv
@mvponlinetv Год назад
Ivi nyinyi wa sanii wa tanzania ndio hamuwezi kuongea bila yakuongea English au inakuwa nihashuo tu
@yusternyirenda7231
@yusternyirenda7231 9 месяцев назад
Dalili zote zinaonyesha zuchu analala na diamond tena kwa asilimia elfu niko paleeeeeee! mapenzi! huwa hayajifichi ipo siku watashindwa kuendelea kuficha 😂😂😂
@ashahamisi5884
@ashahamisi5884 Год назад
Leo sema no no lakini ipo siku utasema yes . Huwezi kuzuia mahusiano kamwe kua siry ficha social media tu.
@mosah2851
@mosah2851 Год назад
Zuchu anasauti huyu mtoto!!
@judithjulius5993
@judithjulius5993 Год назад
Kato kadogo lakini kanaongea point tupu
Далее
КОТЯТА НАУЧИЛИСЬ ГОВОРИТЬ#cat
00:13
🔴LIVE: ZUCHU NA ANJELLA KWENYE LAVIDAVI
30:44
Просмотров 35 тыс.
zuch new challenge
1:31
Просмотров 45 тыс.
Salama Na NANDY Ep 53 | MNOGESHAJI PART 1
35:35
Просмотров 325 тыс.
КОТЯТА НАУЧИЛИСЬ ГОВОРИТЬ#cat
00:13