Ukiangalia sheria zetu it's like they discourage self-employment of any sort. Matokeo yake ikitangazwa nafasi ya kazi 1 wanakuja watu 200 kuomba,hakuna ajira mpya zinazotengenezwa na sekta binafsi. Wazalishaji wadogo walitakiwa kuwezeshwa sana ili kuisaidia serikali kuzalisha ajira.
Tunaiita Dar kuwa ndiko Tanzania huku mikoani ni Tanganyika! Wanafanya wanachokitaka. Kwa mfano Manispaa inataka kujenga soko , inakupa eneo unajenga banda kwa sh Million 5 mpaka 40! Unaambiwa uendeshe biashara kwa kulipa elfu 25 kwa miaka 6 na baada ya hapo miliki inaamishiwa kwa Manispaa, ambaye sasa ataweza kukupangisha au kumpangisha yeyote. Wafikirieni wananchi. Manispaa zisitumie ardhi kuwanyanyasa wananchi
Ukweli ambao hamuwezi kuukubali ni kwamba 'Industrial Revolution' ni mkakati wa siri wa nchi husika. Nchi zote zenye viwanda hawakuamka asubuhi tu wakaanzisha viwanda. Unaomba msaada ukajenge kiwanda wakati masharti ya mkopo hayaruhusu? maybe someone, some day will change the mindset...mtafanya sana mikutano na maombi ila tusipokaa kama taifa na kuanzisha viwanda ambavyo kwanza ni primary producers wa mahitaji ya viwanda vikubwa tutaishia kusafirisha malighafi nche ya nchi. Sera ya viwanda na uchumi haikushirikisha mawazo ya watu wenye entrepreneurship skills, ni watu walikopi au kukaa ndani wakajifungia. hatutazalisha hata nchumvi ya mawe...
@@JuliusMlengeswa waziri anaonyesha njia na kuweka mipango ya kulinda viwanda akiwa huku analalamika tu hawezi kuchukua hatua weye hujui kwa sababu si mzalishaji weye ni mchuuzi nadhani
Sisi wenye viwanda tunajua mapungufu ya vingozi juu ya uchumi waviwanda ni prosser maarum unatakiwa ifutwe ukiwa mchuuzi utapangiwa bei na wenye viwanda na nchi Haiti na fedha za kigeni mpaka wananchi ikiwa hakuna xpot input uchuni utakuwa wa kubatisha
Nahisi kuna kitu hakipo sawa kwenye system zetu na kikubwa ni kwamba ao walioko juuh wengi wahaelewi biashara nin nin na jinsi gani mfanya biashara anateswa na hizi kodi. Ni wakati sasa tukae na tutafakari jinsi ya kulipeleka taifa mbele. Mungu Ibariki Tanzania 🇹🇿
Kwa tanzania ukitaka kufanikiwa tafuta namna ya kukwepa kodi...nazungumza kama mfanya biashara kwa uchungu...unafanya biashara na huku unalipa kodi zinazo fanana ...sevice levy at the same time TRA huo nibmfano. nchi hii ukitaka kuendelea usirasimishe biashara yako kamwe...ni vitu vya hovyo mno na serikali inajua haswa uovu unafanywa na wizara tofauti...sasa unajiuliza ni shule gani hi wanaenda kuendesha nchi kwa namna hii...kila unapojarbu kunzisha biashara ni changamoto za hovyo...jaman wa atendaji wa serikali badilikeni akili za namna gani mnatumia jamani..?
Tatizo la Mama anawapa uwaziri watu sio hawana Vision sio lazima mtu awe ccm huo ni ujinga tunataka mtu mwenye vision kama Masoud huo mduara wa kupata lesen ya biashara it’s too much unalipia nusu na robo ya msingi wako wa biashara kabla ya kupata lesen .Mama Samia Leta watu Dubai waje wasome vipi Serikali zao zimejipanga Katika masuala ya kodi Dubai siku moja tu au mbili unapata lesen hakuna longolongo Mama Samia una Mawaziri mizigo hebu changamka kdg unacherewa sana Dunia inakwenda kasi sana
Huyu dada anasemea juu ya kodi eti "....sasa hivi wameanza kutujia kwa njia nyingine..", hajui kwamba ni Waziri akiwa sehemu ya Serikali ndiyo wametunga hizo sheria ambazo zinavifanya hivyo vyombo vilivyoanzishwa na serikali yenyewe "kuja kwa njia hizo nyingine" za kuhakikisha kuwa hizi SMEs zinaminywa ktk kulipa huo ushuru na kodi? Anadhani anazungumza na chombo tofauti na serikali!! Hapo ndo wenzetu majirani wameona ni siasa hivyo tuwatingishe wawajibike ktk matumizi ya kidogo kinachopatikana na siyo kumnyonya mwananchi na mlipa kodi!! Tubadilike tujue watesi wetu kuwa ni hao tuliowapa madaraka ya kutuongoza ndo wanapofika huko wanajali vya kwao posho na magari ya anasa!
Wananchi wanatumia akili na maarifa mengi kubuni na kuendesha biashara, badala ya kusaidia hawa wenzetu wanatafuta kila njia kukusanya ili wajilipe mishahara mikubwa. Siku za nyuma magari mengi yalikuwa ya serikali (ST), sasahivi magari mengi ya kifahari mitaani ni ya watu binafsi wengi wao wafanya kazi serikalini.
Daaah ni wakati wa serikali kusuport hizi small industries ili waweze kuzalisha zaidi then walipe kodi sio unaanza tu mikodi mixer tozo kibao kwakweli inaumiza sana asee
Na kwa kweli si policy peke yake. Pia inatakiwa budget maalum ya Serikali ku saidia start ups. Zisukumwe na Serikali. Ndio Nchi nyingine zinefanya hivyo
Kiukweli kama kutakuwa na dirisha moja la ulipaji kodi wengi wataipa serikali kodi tena bila shaka maana mm ata kama nina kigari changu nikaambiwa kodi yangu ni 100000 mwaka mzima apo kila mtu kashajikatia chake kuna shida gani sisumbuliwi ila ao wanaopenda kuyafanya mambo yanakuwa magumu ili kujipatia rushwa wanakera
Tatizo ni mama muongeaji baadanya Masudi Amejikita kwa wanawake tu sijui hii dhana wa wanawake kijibagua kwa ila kitu inatoka wapi" Kila kitu mwanamke mwanamke Masud kaongea hajasema wanaume hata sentens moja lakini mama kaingia kutetea wanawake 'basi wangeandaa mkutano wa wanawake . Kweli hii haipendezi kabisa wote hapo ni wazalishashi hakuna jinsia 'kodi"tozo wala soko la wanawake pekee.
Ameniboa sana yule Mama,wao kila sehemu wanaleta siasa za jinsia tu hadi kero. Kipanya anazungumzia nafuu kwa wote yeye anakazana wakina Mama hivi wakina Mama vile,hovyo kabisa.
Ukweli upo kwenye ushindani sisi na majira Zetu. Tz angalia vitu kama chunvi, sabuni. Kenya kwa kiasi kikubwa kwa soko letu. Angalieni malighafi bei zake. Ni kikwazo chetu.
Wekeni kiwango kimoja.mfanyabiasha aambiwe ukitaka kufanya biashara fulani.utalipa sh kadhaa kwa mwaka. Sio kodi kila kona. Mbaya zaidi mnatoza kodi kwenye mauzo ya jumla badala ya faida. Yaani mtu hujaanza biashara unatakiwa ulipe kwanza kodi.
Hakika Tz NZIMA ni MACHINGA WA NCHI ZINGINE HASA ZA UTURUKI ,NA CHINA MPAKA MABILIONEA NAO NI MACHINGA NCHI NZIMA AAAA HAKIKA TUNATAKA KWENDA KWENYE VIWANDAAAAA SIYO KUWA MACHINGA NCHI NZIMA AIBU
Hiyo ndo serikali yetu wanapeleka miswada bungeni na wabunge kwa maagizo ya ccm wanapitisha kisha mwananchi anaanza kulia!! Kesho hao hao wanarudi kuomba kura ili wawndeleze sera za kuminyana kutukamua ili kufadhiri maisha yao huko juu!