Naomba nishauli kitu kuwa zipangwe sheria abazo zinaelekeza kuwa kuzuia kuisogelea hiyo leli ila mtu yoyote akionekana jilani na leli achukuliww hatua kali ili iwe fundisho
Hili lipewe kipaumbele sana na kamati ya ulinzi kwani hawa ni wauwaji sio wezi tu kwa maana mwendo wa chombo hicho ni umeme sasa akitokea mjinga mmoja wa kuharibu hayo unadhani ataathiri raia kiasi gani hasa pale wanapokuwa ndani ya safari. MMh hapana jamani hatakama eti kisingizio maisha magumu katu huwezi rahisisha maisha yako kwa ujinga huo wa kuandaa hatari kwa wenzio. hili hapata tuwe pamoja kwenye kuulinda miundo mbinu yetu hii kwa hali na mali
Zitungwe Sheria Kali Sana za kulinda miundombinu ya Reli ikiwa mtu anapatikana na hati apigwe kufungo Cha maisha Gerezani na kazi ngumu ili iwefundisho kwa wengine.
Hao sio wezi, ila wametumwa na wamiliki bus na maloli,,, tunapaswa kua makini sana, maana isije ikasababisha madhara makuu sana, watu waogope usafiri wa TREN.
Hao watu Wana mcezea Simba sharubu hivi Sisi watu weusi vichwa huwa vina nini nikuwaonyesha mkono wa chuma kuogopa hiyo miundo mbinu kama ukoma serikali iweke camera za Siri sehemu muhimu pia itasaidia.
Hivi unajua maajabu bado hayajaisha duniani hasa Tz ni aibu na ajabu sana hivi watu watasarabika lini kutoka kwenye akili ya giza kuwa na akili yenye nuru Yani KODI ZOTE TUZO TOZWA NA MIKOPO ANAYO HANGAIKA NAYO RAIS WETU ILIKUJENGA NCHI IWE NA MAENDELEO MJINGA MMOJA ANALETA......(😂)
Jamani hivi sisi mbona tunavichwa vigumu ,,hatuoni umhimu wa reli mpaka mtu anaenda kuharibu reli,,,muwakamate mkawafunge ili liwe fundisho kwa walio na tabiazo
Sisi wazungu wanatuletea HAKI ZA BINADAMU, mbona China ukifanya uharifu wa aina yoyote unapigwa chuma hadharani, sisi Tanzania utasikia haki za binadamu, hizo haki za binadamu ndo zinalinda uharifu.
Hawa ni watu wasiojitambua kizazi cha laana siyo kinapinga maendeleo ya mtu fulani. Wizi na uhalifu siyo itikadi au mtaji wa kisiasa. Ni vema wapatikane ili ionekane hukumu yao kama itacheleweshwa au kuachwa tu kama za watuhumiwa wa ripoti ya cag.
Kamata na ning'iniza kwenye kamba hawa ndiyo wanastahili kuwekwa kizuizini zaidi ya hawa wanaotekwa na kupotezwa!! Fungeni camera hata kwenye vilima vyote morogoro, aidha jkt wapo wawekeni kwenye hii njia. Suala la kusifia mtu ni uchawa jitahidi kuiepuka fanya kazi kwa ajili ya watanzania ndiyo wanaohitaji maendeleo ni siyo mtu!