Wafanyabiashara Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma kuanzia Jana May 29, 2021, walianza mgomo wakiwatuhumu baadhi ya Maafisa wa TRA kwa kuwabambikia kodi Wafanyabiashara wasiotoa rushwa kwao.
Kwenye mgomo huu Wafanyabishara hao wamesisitiza kwamba waofisa waTatu wa TRA waliowataja majina na wanao waobambikizaji woondolewe Mara moja kasulu hawawataki kabisa.
Chama cha Mapinduzi Wilayani kasulu kupitia kwa mwenyekiti wa Chama Mbelwa Abdallah amesema Chama kinaunga Mkono wafanyabishara kwa kigoma kutofungua maduka kutokana na manyanyaso hayo ya TRA.
Ameyasema hayo mbele Mbunge wa Kasulu Mjini Prof. Joyce Ndalichako pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye wakati wa Mkutano na wafanyabishara waliogoma.
30 май 2021