Тёмный

Sallam Afichua Walichokifanya WCB Baada Kufungiwa Na Media Zote Kubwa | SALAMA NA SALLAM SK PT 2 

YahStoneTown
Подписаться 395 тыс.
Просмотров 87 тыс.
50% 1

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Sallam Sharaff ni lejendari, na hilo liko wazi kwa anayetaka na asiyetaka, kwa umuhimu wake kwenye maisha ya msanii nambari moja kwa sasa ni kama nywele, usipomkuta kichwani basi hata kwapani hatokosekana. Na kwa utashi wangu nadhani kama wana Bongo Flava au wasanii ambao ‘wako tayari kuwekeza’ basi wangemkimbilia kwa kasi ya 4G ilimradi wapate mawazo tu ya jinsi gani wanaweza kufanya ‘meli’ yao ifike na pale panapotokea mrama wajue wimbi gani la kuliepuka na wimbi gani ndo walipandie kwa juu.
Sallam si muongo na hili ninalijua kwasababu ni rafiki yangu, atakavyokuambia ndivyo lilivyo, Sallam anapenda pesa na hilo liko wazi na wala hajifichi nalo ila kubwa zaidi Sallam anapenda MAENDELEO. Ukitaka msielewane naye milele na milele basi onyesha nia au muonyeshe moja kwa moja kama unataka ’kumharibia’ mkate wake. Hakika hatokuacha salama. Atahakikisha unaenda na maji kwasababu mkate wake ndo maisha yake. Tofauti yake na wengi wetu ni kwamba wengi wetu tukijua mtu anataka kukuharibia basi na wewe utajificha au utamuepuka au utamchukia tu, Sallam yeye atakuonyesha waziwazi kama HAKUPENDI.
Muziki anaufahamu vizuri tu na mengine anayang’amua as we go kama binadamu wa kawaida, mapenzi yake kwa mziki huu na kwa kupenda anachokifanya ndo kunamfanya awe THE BEST MANAGER. Maisha na mipango na maendeleo ya msanii nambari moja kwa sasa yalianza kubadilika sana mara baada ya Sallam kuingia kazini, na ilibidi aanze kama International Manager maana kwa upande wa ndani tayari Babu Tale na Said Fella walikua washapatawala. Haikua kesi kwake, ambacho alikifanya ni kuhakikisha Diamond anapata collabo na show nyingi za nje ambazo yeye alikua anaenda naye. Wakati akiwa wanapokua alitumia nafasi hiyo kutengeneza network nyengine. Mipango yake na uwajibikaji na jinsi vitu vilivyokua vinasogea vilimfanya Platnumz ampende zaidi, amshirikishe kwenye mambo mengi zaidi ambayo matunda na malipo yake ndo haya ambayo wanakula leo na kesho na keshokutwa ilhali mimi na wewe tunashuhudia historia inavyozidi kuandikwa.
Kwa Said Fella kupata udiwani nako pia kulimfanya Sallam apate majukumu zaidi ya hata ya ndani sasa maana kipindi kile cha Hayati JPM kazi ilikua inabidi ifanyike na Sheikh Said alipigiwa kura na watu, so mara nyingi ilikua inabidi afanye kazi za kutumikia wananchi wake, na huku nyuma Sallam akawa anaezeka banda lake la kuishi kwenye ufalme wa Diamond Platnumz.
Nakumbuka mwaka 2018, London Town, Diamond alimaliza show zake na Sallam akabaki nyuma, kilichowapeleka kule ilikua ni show ambayo yeye Sallam, my cousin Dulla Meru na moja ya mapromota hodari kutoka Nigeria ambaye anaishi London Ndugu Smed waliiandaa, ilienda poa na naamini ile ilifungua milango mingi sana. Alibaki nyuma kuhakikisha mambi yote yanakwisha freshi na pia kutengeneza network nyengine kwa matumizi ya baadae. Alibaki nyuma na mimi. Tuli enjoy, tuli jifunza na pia yeye aliweza kuweka MIZIZI yake vizuri ili mbuyu huu tunao uona leo usimame.
Mawe mengi mno kapigwa. Maneno mengi sana yamesemwa juu yake, kama binadamu hawezi kuwa amekamilika au kamaliza, ila jitihada zake na kazi ambayo anaifanya inabaki inamzungumza kwa niaba yake. Kama ambavyo yeye anasema, kwanza yeye ni MFANYA BIASHARA, mengine yanakuja baada ya hapo. Diamond anamlipa Sallam kwa asilimia kila mara anapoleta BIASHARA kwenye MEZA YAKE. Faida ni ya WOTE. Sio mmoja ananenepa na mwengine anakonda kama ilivyo kwenye mahusiano mengi ya biashara hapa nyumbani na pengine Afrika na duniani kwa ujumla.
Ukiniuliza mimi nitakuambia, hapa kuna mengi ya kujifunza.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪RU-vid Link bit.ly/RU-vidSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Развлечения

Опубликовано:

 

24 июл 2022

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 215   
@edsonjeremiah5905
@edsonjeremiah5905 2 года назад
Sipendi marafiki Ila nahitaji wafanya biashara wenzangu that's big point Salam salute.
@azamzahoro6548
@azamzahoro6548 2 года назад
"Mimi sina rafiki mimi ninawafanyabiashara" unyama ni mwingi sana.
@Igauf3
@Igauf3 2 года назад
Great point, look at the top 100 of all African countries on Apple Music et al. You will agree with Salaam’s point the market reflect to what he is saying. Only, Northern African countries have high numbers of their musicians in those list.
@nsaluhenry6435
@nsaluhenry6435 2 года назад
Jamaaa anajua kuongea asee wasanii muweke heshima jamaa atawafikisha mbali Big Up SK
@Valdo.Suleiman
@Valdo.Suleiman 2 года назад
Duh yani huna marafiki wala huitaji marafiki kweli we mwamba😁😆
@allahisone6386
@allahisone6386 4 месяца назад
SALLAM NI LEVEL NYENGIN
@UlimeA
@UlimeA 2 года назад
Hii jamaaa inawaza PESA tu.🙌 big up
@bongelabwana7523
@bongelabwana7523 2 года назад
Mwamba Salam hapa duniani hakuna marafiki wengi wanafiki sana wakiona una hela kidogo wanajisogeza , harmonize alipokua ananuka vikwapa hakuna aliyekua anajali wala kutaka kumsaidia, leo katoka anapata hela na mademu kila mtu anajifanya anampenda . bindadamu WANAFIKI kinoma noma
@taarifahabari4856
@taarifahabari4856 2 года назад
Nani aliye mtoa?
@roqerz
@roqerz 2 года назад
This man is businessman
@3kings63
@3kings63 2 года назад
Nakubal sana📢🥰🔞🧡 Marafik wanga tuu
@paulmbonika2459
@paulmbonika2459 2 года назад
Napenda 'Kujiamini' kwa Salam SK, Big up, one of the people i would love kukutana nao FACE TO FACE niweze chimba madini mawili matatu.
@rajabdibwa6415
@rajabdibwa6415 2 года назад
This guy is a good businessman
@geoffreybasesa2015
@geoffreybasesa2015 2 года назад
Sipendi kuhulizwa maswali, so direct and straight forward salama. Keep it up miss
@mrmakungaone321
@mrmakungaone321 2 года назад
Sallama hongera kwa kazi be blessed SK
@yama_virginhairthequeen1065
@yama_virginhairthequeen1065 2 года назад
THE SMART INTELLIGENCE MANAGER no need kuwa na friends oh yeah
@mussachabonga9595
@mussachabonga9595 2 года назад
Absolutely interview,big up sister Salama.
@jumamofu9573
@jumamofu9573 2 года назад
Niliisubiri Sana Hii interview
@Hanskapella
@Hanskapella 2 года назад
Show imekua Fupi Sana, Kuna Mambo mengi Sana yakuongea na Sallam Sk. Anamadini mengi Sana huyu mwamba.
@teggertegger3669
@teggertegger3669 2 года назад
Big up SK kuazia leo nimekukubal salute 👏👏👏👏👏👏👏👏🍾🍾👑🤣🏃‍♂️🏃‍♂️
@iammichaellukindo
@iammichaellukindo 2 года назад
Everytime ukimsikiliza salama unajifunza upya
@mussamsella8560
@mussamsella8560 2 года назад
Naapa ....Najiona sahihi kwa mengi sana. Biashara ina mambo mengi sana,hawa watu wanawekeza wanawekeza muda,pesa,na akiri zao halafu wewe unataka usaidiwe kwa huruma ya maneno.Hili haliwezekani hata kidogo.
@msangodiesel3132
@msangodiesel3132 2 года назад
Jamaa kaongea point Sana
@BuraK-bk9iw
@BuraK-bk9iw 2 года назад
*ila huyu jamaa ni kichwa asee 😂😂😂 hapa Diamond platnumz kapata meneja asee* 😂😂😂
@henryedmund1046
@henryedmund1046 2 года назад
That was life style harmonize issue
@robertmbaga9432
@robertmbaga9432 Год назад
Swali la mwisho zuri sana,Salama itabidi siku moja ujifanyie interview mwenyewe kwasababu unauliza vizur sana maswali nahisi hakuna anaekushinda.Halafu naomba niletee Alex Luambano wa Clouds
@murschasser5503
@murschasser5503 2 года назад
Interview ya salama ni borrra 👏
@moodymachinga8008
@moodymachinga8008 2 года назад
Mendez Nimependa sn hii interview brother big up sn
@nahyialetomia9284
@nahyialetomia9284 2 года назад
Akili kubwa Mendez
@alphamgimba7125
@alphamgimba7125 2 года назад
Jamaa anaakili san
@mfalmekaitaba2425
@mfalmekaitaba2425 2 года назад
#Sallam ahsante kwa interview kali sana.
@edwardokumu8453
@edwardokumu8453 2 года назад
I feel like interviewing somebody like sallam you need more time..there were many issues about harmonize that were not asked e.g allegations he made at the airport,also issues around the exit of rayvanny and hanstone..
@yama_virginhairthequeen1065
@yama_virginhairthequeen1065 2 года назад
Let rat remain in the hole😒
@davidmwombeki5410
@davidmwombeki5410 Год назад
P
@davismakule5965
@davismakule5965 2 года назад
Jamaa anajibu maswal vizur sana, straight forward
@erickmichaelmugele2107
@erickmichaelmugele2107 2 года назад
Vijana wengi wakiweza kuiga mindset kama ya Sallam SK watafika itakuwa vizuri sana...
@byaminarehema6745
@byaminarehema6745 2 года назад
Is so real !
@yohanakaini
@yohanakaini 2 года назад
one thing i like about SK is that the man is real, hajui ku fake yan black is black
@phranklynpius9478
@phranklynpius9478 2 года назад
Ninachokubali kuhusu hii shoo, yanaulizwa maswali yenye majib 'uncomfortable'....bonge la podcast!
@othinielkamyola3697
@othinielkamyola3697 2 года назад
Nomaaaàa sana sallam
@brunofernandez6608
@brunofernandez6608 2 года назад
The man talk the truth
@sheilanyahoza5633
@sheilanyahoza5633 2 года назад
HUU NI WAKATI WA MOND SASA ....WE NEED HIM
@mumaheza151
@mumaheza151 2 года назад
Diamond
@calvinloveambroce842
@calvinloveambroce842 2 года назад
Bonge la interview ever huyu sallam ni intelligent sana
@nsabiyaremyezacharie6387
@nsabiyaremyezacharie6387 2 года назад
Mendez kama Mendez
@emmanuelcaliph3714
@emmanuelcaliph3714 2 года назад
Salam sk big up sanaaaaaaaaa
@sleeprelaxation8431
@sleeprelaxation8431 2 года назад
i like him🤣wao waseme sisi tunaenda kweli kweli
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 2 года назад
someone OG that's sallam SK Mendez 🤣🤣hataki unafiki
@rajabdibwa6415
@rajabdibwa6415 2 года назад
He is straightforward person!
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 2 года назад
@@rajabdibwa6415 yap
@hassanikobelo3688
@hassanikobelo3688 Год назад
Salama is best and first presenter in Tz and east africa since day one no cap
@ibrahimkibira9943
@ibrahimkibira9943 Год назад
Salama your international for really 😘 may God bless you 🙏
@CROWNMEDIAKE
@CROWNMEDIAKE 2 года назад
Hii nimependa sanaaa
@nassibsaid1348
@nassibsaid1348 2 года назад
Nimekuelewa sana salam
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 2 года назад
🙌
@MasterChief-Ortiz
@MasterChief-Ortiz 2 года назад
sk hakuwa na njaa nin
@King-Buda
@King-Buda 2 года назад
Bless
@bintyaroy6734
@bintyaroy6734 2 года назад
Safi
@egnokapinga16
@egnokapinga16 2 года назад
Boss Mendez akili mingi sana. Anajua🙌
@ayubukassim7995
@ayubukassim7995 2 года назад
Nakubali hiki kipindi very 🔥🔥🔥🔥
@daudiraston747
@daudiraston747 2 года назад
Big man congrats
@paulineonkoba5792
@paulineonkoba5792 Год назад
I love Salam his business oriented
@franciskyombo9394
@franciskyombo9394 2 года назад
Sk Multigenius
@fundiwamoldzapevingblock6378
@fundiwamoldzapevingblock6378 2 года назад
Umetisha Sanaa sanaaa sk nakubariiiii sanaaaa
@mtaostephen3660
@mtaostephen3660 2 года назад
Ukiwa mnafiki huwez kumuelewa
@Kobe_254
@Kobe_254 2 года назад
Hapo mwamba aksema ukweli... Tamaa ndio inasumbua wasanii, hilo nalifahamu... ata Rayvanny bado ni tamaa, ila tamaa mwisho wake mbaya sana... Ona Harmonize sahivi ana mihela na Range Rover, kajala atamlamba ata mkundu... mmakonde!! mumngu kamsaidie!!
@HallyTunchy
@HallyTunchy 2 года назад
We need a Salama na Platnumz Podcast And Harmonize Too✈️
@abdulraufmohammedsalum6806
@abdulraufmohammedsalum6806 2 года назад
Wa kwanz
@mountaincoffee7
@mountaincoffee7 Год назад
Mlete jamaa wa radio one wa habari nyepes
@ramayonline2281
@ramayonline2281 Год назад
Salama na Diamond Platnumz next
@bigELLY-zz7tw
@bigELLY-zz7tw 2 месяца назад
Yeah don Mendez🎹🎹
@nsaluhenry6435
@nsaluhenry6435 2 года назад
Wasafi itaendelea kuwa juu kwa menejas walionao jamaa yupo really anajitambua sana
@shangwerobert5639
@shangwerobert5639 2 года назад
I like this guy
@kashungamagohe2659
@kashungamagohe2659 2 года назад
Interview ya salama.swal zur sana
@nishaabdula5015
@nishaabdula5015 2 года назад
Ht mm sipokei mkono. Wk ss msibani NDO nn kila. Kwani slm ndo mfiwa au korosho alitaka Kiki ndo maana alifanya vile
@reisezone4574
@reisezone4574 2 года назад
namuelewa salaam bongo ukiwa na misimamo utetereki sio mnafiki lazima uchukiwe ndio kinachomtokea salama yuko straight msimamo hayumbishwi ndio maana anachukiwa
@rajabdibwa6415
@rajabdibwa6415 2 года назад
Wabongo ukiwachekea sana watakupanda kichwani ndio mana Saĺlam hana marafiki
@UlimeA
@UlimeA 2 года назад
Huyu jamaa kwenye issue ya business ni makin sana
@yusuphwilliam5343
@yusuphwilliam5343 2 года назад
Salam maswali yako mazuri sana
@zurrychannel235
@zurrychannel235 Год назад
Good interview
@subirajohn728
@subirajohn728 2 года назад
Diamond❤️❤️❤️
@thomaslyimo1729
@thomaslyimo1729 2 года назад
He is mastermind
@aaronernest3752
@aaronernest3752 2 года назад
#Mogul 🔥🔥🔥
@mao9622
@mao9622 2 года назад
Boss Mendez
@cossangraphix6843
@cossangraphix6843 2 года назад
Nice interview
@johanakunambi6975
@johanakunambi6975 2 года назад
Good
@michaeljeremiah5364
@michaeljeremiah5364 2 года назад
Dada angu salama niweza pata angarabu nafasi nipige na ww pic tu....dada 😭
@mirromsodoki2777
@mirromsodoki2777 2 года назад
Ilauyo jamaa niatali 😂
@jamesngalijah3710
@jamesngalijah3710 2 года назад
nakubali sanaaaa
@foteliberty4080
@foteliberty4080 2 года назад
Waiting for Kitenge.
@tanzania2559
@tanzania2559 2 года назад
Business, Mimi sina haja ya kukutana na sk ila he is a business minded
@salomesamson6904
@salomesamson6904 2 года назад
Hamonize mibangi yule aache mibangi yule mibangi yake ndo inamharibu hamonize
@archbordygodfrey2614
@archbordygodfrey2614 2 года назад
Jamaa anasauti kama ya ridhiwani kabisa
@pirato5462
@pirato5462 2 года назад
Boss kama boss
@muunganomapunda8440
@muunganomapunda8440 2 года назад
Salama aende The Joint
@babalaujamaa7131
@babalaujamaa7131 2 года назад
Mwambaaaaa huyu hapaaaa ✌️✌️✌️✌️
@ibrahimfarha3853
@ibrahimfarha3853 2 года назад
N'a base n'a kuskiliza WCB tuuuu
@abdallahmdangadachi7030
@abdallahmdangadachi7030 2 года назад
Sijawahi kusikia kuhusu hiyo inshu ya Mombasa hapa ndonimejua leo. Lkn inaonekana kweli Salam alienda kuchafua hali ya hewa. Miaka kadhaa nyuma King alikua na show kwenye tamasha moja kubwa la mziki Zanzibar stonetown kwenu Salama. Kipindi hiko D alikua na mazaa wa Uganda. Basi wakati king anafanya yake jukwaani D alienda na mazaa wake forodhani kula urojo. Salama unajua umbali wa foro na lile jengo kwenye buku mbili. Ilikua tafrani maana washabiki hawajui waende wapi
@bukuruyassini
@bukuruyassini Год назад
Ndo Boss Boing
@romakoko2292
@romakoko2292 2 года назад
Interview ya zuchu iko wapi
@chunanachu2529
@chunanachu2529 2 года назад
Salam mtu mzuri ukiwa mnafki ndio utamuona anazingua .....but very straight guy👊
@sportingtv7159
@sportingtv7159 2 года назад
hii kichwa ni noma big up sana sallam😂❤
@vincentkiprotich7959
@vincentkiprotich7959 2 года назад
Sallam is real!
@hbboe1849
@hbboe1849 2 года назад
Uyu ndo mwamba sasa...😂😂
@theodoreconstantine2565
@theodoreconstantine2565 2 года назад
ok
@egnokapinga16
@egnokapinga16 2 года назад
BossMendez
@siaammo1104
@siaammo1104 Год назад
jamaaa ana jiamini hatariiiii
@sheemsuka4019
@sheemsuka4019 2 года назад
Tuletee Harmonize basi
@user-sp3gg7id8q
@user-sp3gg7id8q Год назад
Alikiba anatchokwama ni views na consistently ya kutoa video za nyimbo haraka haraka kila mwezi kama mondi, hizo views haziji kwa fans tu, unaboost ili uonekane umefanya vizuri iyo season /12 months hii itamfanya apate nomination kwenye awards za nje ya nchi na kualikwa kwenye matamasha mbali mbali. Pia views ni ghali that's why mondi hana hata nyumba ameinvesting sana huko akipiga shows anaenda kuboosti ili ashikilie position ya juu.
@salmadulazi6876
@salmadulazi6876 2 года назад
Hiv ile salama na Salma Msangi imeishia wapi mbona kila nikifungua nakutana tangazo tu kulikoni?
Далее
지민 (Jimin) 'Who' Official MV
03:28
Просмотров 12 млн
This or That 🛍️
0:52
Просмотров 3,4 млн
Продал не тот порошок... #shorts
1:00