Aaaah aaah! Mama adija jiandae 😂😂😂.Huyu Mzee namkubali sana muongeaji na mcheshi. Lakini wafanye mpango wamuwezeshe mzee hata basi wamjengee nyumba nzuri hata ya chumba kimoja maana anajari sana maendeleo ya wengi kuliko ya kwake mwenyewe.Mungu amjalie sana mzee na mtani wangu Waziri Bashungwa 🎉🎉🎉
Mhe. Bashungwa Mungu akubariki sana. I am so overwhelmed indeed. Ukigusa maisha ya wahitaji basi Mungu naye hushughulika na maisha yako pia. Glory to God 🙏
Mh. Bashungwa na Mzee wa Jogoo Hongereni sana. Mnasaidia sana kutuunganisha wananchi na serikali yetu. Mh. Bashungwa Mungu azidi kukulinda, na kukuongezea hekima na busara katika utendaji wako.
Tuna watu wazuri sana katika hili Taifa ila wamefungwa mikono!!! May the Living God bless you Hon. Innoocent Bashungwa. Nimebarikiwa sana kwa kuona Makazi ya Mzee wetu!!!
MHE. BASHUNGWA nakupongeza sana kwa kumtembelea Mzee KIMBWEMBWE a.k.a. Mzee wa Jogoo wa Somanga- Kilwa huko mkoani Lindi.Hakika Mhe. Waziri BASHUNGWA nakuombea kwa MWENYEZI Mungu akubariki sana kwa kujitolea kutaka kumfanyia "JAMBO" la "UJENZI WA NYUMBA YA KUISHI" baba yake "RAIS".
Haya yote tunayoyaona ni matunda j.p.m ameliacha Taifa na viongozi wenye upendo,nahuruma, bashungwa, na makonda mungu awalinde sana endeleeni nahuo moyo matunda mutayaona
Dah mzee yuko vizuri namkubali na Bashungwa Mwenyezi Mungu akubariki ubadilishe maisha ya huyu mzee hiyo dua sio ndogo imemfikia Mwenyezi Mungu haina unafiki wowote imetoka moyoni haswaaa
Masha allah nmeisklza hii video hadi namhisi huyu mzee natamn angepew nyumba nzuri tu apo apo na sio kujengew tu kw sbb utachlewa ujenzi kutokana umri wake...allah amhifadh na amjaalie umri mrefu aamn ya rabbal almn❤
Mama Yangu Samia tambua unamajembe Yafuatayo: Jerry Silaha, Bashungwa, Biteko. Hii ni Kwa Mawaziri.Sifamu kama Kuna mawaziri wengine. Ila kama itakupendeza. Dorothy Gwajima arudi afya. Madudu ni mengi mama yangu.
Bado tunao watu wema na huruma kwa jamii makonda ali hapi jerry silaa biteko majaliwa bashungwa doròthi alikuwa anajali sana MUNGU awainue zaidi katika kulitumikia taifa lenye viongozi wenye ubinafsi
Nimeipenda sana ziara ya namna hiii Mh. Waziri pongezi kwako kwa kumtembeleaa mzee huyu na kumjulia hali nyumban kwakee na kujionea mazingra anavyoishi pamoja na familia yake.., viongozi wengine igeni mfano wa namna hiii msipite barabarani na misafara yenu hiyo haitoshii watembeleeni hata wananchi majumbani mwao mwone maisha halisi
Mheshimiwa Bashungwa ni kiongozi wa aina yake, ana unyenyekevu wa hali ya juu, hana majivuno, haweki cheo mbele. Ubinadamu uko mbele. Mungu amjalie uzima, hekima na uzima.
Mungu akuzidishie waziri bushungwa umefanya kitendo cha kiungwana sana na mzee mbwembwe ni mmoja wa wazee wenye busara sana mungu akuweke inshala ntafunga safari kuja kukusalimia kunako na majaaliwa sisemi lini lkn ntakjja inshala
Si vyema ,tukawa tunafurahia uhuru wa inchi hii mbila kukumbuka mikoa na maeneo yaliyo pigania uhuru kama vita vya majimaji maeneo hayo yanahitaji kuboreshwa sana.
Mzee Kimbwembwe anafahamu vizuri historia ya hivyo vita kwa sababu ilianza maeneo hayo hayo ya Kilwa wanapoishi na mababu zao ndiyo walioianziaha hiyo vita. Cha kusikitisha wajanja wachache wamebadilisha historia kwa kuandika uongo eti imeanza Songea jambo ambalo sio kweli. Vita iliratibiwa Kibata na chokochoko ya kumuinguza vitani mjerumani waliianzishia Somanga maeneo ya Simu kwa kufyeka mashamba yao ya pilipili na pamba na kuwaua askari wa kijerumani hapo Somanga kwenye boma lao ndipo wajerumani wakakasirika wakatuma jeshi na mapigano yakaanza rasmi na kuenea kusini kote hadi Songea na maeneo ya mkoa wa Pwani na Morogoro.